![]() |
Ofisa Mkuu
wa Biashara wa Zantel, Sajid Khan (kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Michezo,
Leonard Thadeo na Meneja Mkuu wa African Lyon, Rahim Kangezi ‘Zamunda’ wakati
wa kutangaza dili la oleo mchana.
|
Na Mahmoud Zubeiry
KLABU ya
African Lyon imezuiwa kuweka mabango yake kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
wala kuvaa jezi zenye nembo ya mdhamini wao, kampuni ya simu ya Zantel katika
mchezo wa leo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Simba SC.
Mida hii, BIN
ZUBEIRY imeshuhudia kasheshe baina ya wafanyakazi wa Uwanja wa Taifa,
dhidi ya viongozi wa African Lyon.
Ikumbukwe leo
mchana, Lyon imetangaza kuingia mkataba wa udhamini na Zantel wa miaka mitatu
na inatarajiwa kuanza kuutumikia katika mchezo wa leo wa ufunguzi wa Ligi Kuu
dhidi ya Simba, utakaonza saa 10:30 jioni.
Meneja Mkuu
wa Lyon, Rahim ‘Zamunda’ Kangezi amesema msimamo huo wa kuzuiwa kuvaa jezi za
mdhamini wao na kuweka mabango utaendelea, basi wao hawatacheza mechi hiyo.
“Katika
maboresho ya mkataba wa udhaimini wa Ligi Kuu wa Vodacom, hili
limekwishazungumzwa na limerekebishwa kwamba klabu zitaruhusiwa kuingia mkataba
na kampuni nyingine za simu.
Pia, leo
katika kikao cha kabla ya mechi tulipeleka jezi hizi na zikapitishwa, sasa
iweje tunaambiwa hatuwezi kuvaa, sisi hatukubali, kama hatuvai na hatuchezi,”alisema
Zamunda.
Alipoambiwa
kuhusu kanuni zitawahukumu wasipocheza kwa kushushwa Daraja, Zamunda alisema hawagomei
mechi, bali wanagoma kucheza kwa sababu ya kuzuiwa, hivyo haoni ni vipi kanuni
hiyo itawahukumu, zaidi wao watapambana kupata haki yao na sana mechi hiyo itachezwa
siku nyingine, ambayo TFF watakuwa tayari kuiruhusu Lyon kuvaa jezi za mdhamini
wao.
Mapema leo
mchana, Ofisa Mkuu wa Biashara wa Zantel, Sajid Khan alitangaza kampuni yake
kuingia mkataba wa miaka mitatu kuidhamini Lyon, mbele ya Mkurugenzi wa
Michezo, Leonard Thadeo katika hoteli ya Hyatt Regency (zamani Kilimanjaro),
Dar es Salaam.




.png)
0 comments:
Post a Comment