• HABARI MPYA

    Saturday, September 15, 2012

    ZANTEL WAINGIA MKATABA WA KUIDHAMINI AFRICAN LYON

    Ofisa Mkuu wa Biashara wa Zantel, Sajid Khan akimkabidhi jezi, Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo kwa niaba ya klabu ya African Lyon ya Dar es Salaam, katika hoteli ya Hyatt Regency (zamani Kilimanjaro), Dar es Salaam wakati wa kutangaza kuingia mkataba wa kudhamini klabu hiyo kwa miaka mitatu. Wanaomfuatia Thadeo ni Meneja Mkuu wa African Lyon, Rahim Kangezi ‘Zamunda’ na Charles Otieno, Mkurugenzi wa Ufundi wa African Lyon. Kulia kabisa ni mchezaji chipukizi wa Lyon, Jarufu Magesa, ambaye anapelekwa na klabu hiyo Marekani kusoma na  Kocha Muargentina Pablo Ignacio Velez. Lyon itashuka dimbani jioni hii kumenyana na Simba SC katika mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ZANTEL WAINGIA MKATABA WA KUIDHAMINI AFRICAN LYON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top