• HABARI MPYA

    Sunday, September 16, 2012

    JAMHURI WACHAPWA THALATHA ZANZIBAR, MAFUNZO YABANWA


    Na Ally Mohamed, Zanzibar
    TIMU ya Bandari imetoka sare ya kufungana bao 1-1 na Mafunzo katika Ligi Kuu ya Zanzibar leo kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
    Bandari walikuwa wa kwanza kuliona lango la Mafunzo kupitia mshambuliaji wao Mussa Omar 'Kidishi' katika dakika ya 25 na Mafunzo walisawazisha kupitia kwa Mohammed Abdulrahim dakika ya 52.
    Kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba, Jamhuri ambao ni wawakilishi wa Zanzibar katika Kombe la Shirikisho mwakani, wametandikwa na Chipukizi mabao 3-0. Mabao ya Chipukizi yalifungwa na Muhsin Mohammed dakika ya 11, Faki Maalim dakika ya 21 na 60.
    Ligi hiyo inatarajia kuendelea tena kesho kwa mechi moja Uwanja wa Amaan kwa kuzikutanisha timu za Mtende Rangers na Chuoni.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JAMHURI WACHAPWA THALATHA ZANZIBAR, MAFUNZO YABANWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top