![]() |
Wachezaji wa Yanga |
Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA Mkuu
wa Yanga SC, Mbelgiji Tom Saintefiet amembeba Haruna Niyonzima ingawa ni
mgonjwa katika kikosi chake cha wachezaji 18 wanaondoka leo saa 8:00 mchana kwa
basi kwenda Morogoro, kwa mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,
dhidi ya wenyeji Mtibwa Sugar, kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na amemuacha
mshambuliaji Jerry Tegete.
Wachezaji anaokwenda
nao Moro leo ni makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki Shadrack
Nsajigwa, Juma abdul, Godfrey Taita, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, David Luhende,
Oscar Joshua na Stefano Mwasyika.
Aliwataja
viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Nizar khalfan,
Shamte Ally na Simon Msuva, wakati washambuliaji ni Didier Kavumbangu, Said
Bahanuzi na Hamisi Kiiza, wakati wanaobaki walikuwa ni kipa Said Mohamed, mabeki
Ladislaus Mbogo, Job Ibrahim, viungo Rashid Gumbo, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum
Telela, Omega Seme, Nurdin Bakari, Idrisa Assega, Issa Ngao wa Yanga B anayekomazwa
kikosi cha kwanza na mshambuliaji Tegete.
Huo utakuwa
mchezo wa pili kwa Yanga katika ligi hiyo, baada ya awali kulazimishwa sare ya
bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi.
Saintfiet jana
aliwaomba radhi mashabiki wa Yanga kwa sare ya Jumamosi kwenye Uwanja wa
Sokoine na akawatupia lawama viongozi wa klabu hiyo, kwa maandalizi mabovu.
Saintfiet alilalamikia
kulala kwenye hoteli mbaya, yenye vitanda vichache na vidogo, vilivyosababisha
watu wakalala mzungu wa nne, na chakula kibaya na kwa ujumla alisema hawakuwa
vizuri kabla ya mechi hiyo. Alisema yeye
alilala kitanda kimoja na Louis Sendeu na Mbuyu Twite alibanana na Didier
Kavumbangu na hoteli haikuwa na mabomba vyooni wala bafuni, hivyo kulazimika
kuingia na ndoo na kuogea kata.
Alisema pia
hoteli hiyo ilikuwa katikati ya mji na karibu na stendi ya mabasi, kila alfajiri
kelele nyingi na kwa ujumla timu iliingia uwanjani ikiwa haiku vizuri.
“Mimi kwa
mfano sijaoga siku mbili, kwa kweli tulikuwa katika mazingira magumu na
wapinzani wetu walicheza soka ya kuudhi tangu mwanzo, kupoteza muda, na marefa
hawakuchukua hatua, tulipoteza nafasi kupitia kwa Kiiza (Hamisi) na Msuva
(Simon), siwezi kulaumu mchezaji wangu yeyote, lakini hiyo ndiyo hali
halisi,”alisema Saintfiet.
Baada ya mazoezi
ya asubuhi kwenye Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam na saa
8:00 mchana watasafiri kwa njia ya barabaraba kwenda Morogoro ambako wakifika
watatafuta hoteli nzuri mapema.
Alisema
anajua hata Uwanja wa huko, Jamhuri si mzuri na mechi itakuwa ngumu kwa sababu
Mtibwa Sugar nao walitoka sare ya bila kufungana na Polisi katika mchezo wao wa
kwanza Jumamosi na anaiheshimu timu hiyo kama moja ya timu tano kubwa Tanzania,
pamoja na Simba, Azam na Coastal Union.
“Lakini
pamoja na kwamba Simba wamependelewa kupangiwa ratiba ya kuanza kucheza
nyumbani mechi tano mfululiuzo, nakuambia Mei mwaka 2013 Yanga ndio itavishwa
taji la ubingwa wa Ligi Kuu, acha wafurahie sasa hivi, watalia mwisho,”alisema
Mtakatifu Tom.
REKODI YA SAINTFIET YANGA
1.
Yanga
Vs JKT Ruvu (Kirafiki) 2-0
2.
Yanga
Vs Atletico (Burundi, Kagame) 0-2
3.
Yanga
Vs Waw Salam (Sudan, Kagame) 7-1
4.
Yanga
Vs APR (Rwanda, Kagame) 2-0
5.
Yanga
Vs Mafunzo (Z’bar, Kagame) 1-1 (5-3penalti)
6.
Yanga
Vs APR (Rwanda, Kagame) 1-0
7.
Yanga
Vs Azam (Kagame) 2-0
8.
Yanga
Vs African Lyon (Kirafiki) 4-0
9.
Yanga
Vs Rayon (Kirafiki, Rwanda) 2-0
10.
Yanga
Vs Polisi (Kirafiiki, Rwanda) 2-1
11.
Yanga
Vs Coastal Union (Kirafiki) 2-1
12.
Yanga
Vs Moro United (Kirafiki) 4-0
13.
Yanga
Vs Prisons (Ligi Kuu) 0-0
0 comments:
Post a Comment