• HABARI MPYA

    Monday, September 17, 2012

    NIYONZIMA HATARINI KUWAKOSA MTIBWA SUGAR KESHOKUTWA

    Niyonzima na famili yake 

    Na Mahmoud Zubeiry
    KIUNGO wa Yanga, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima amerejea Dar es Salaama akiwa mgonjwa kutoka Mbeya, ambako Jumamosi aliiongoza timu yake katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, dhidi ya wenyeji Prisons, ulioisha kwa sare ya bila kufungana.
    Kocha Mkuu wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet aliiambia BIN ZUBEIRY jana baada ya kutua Dar es Salaam kwamba wachezaji wote 20 aliokwenda nao Mbeya wamerudi fiti, kasoro kiungo huyo wa kimataifa wa Rwanda pekee, ndiye ‘anaumwa sana’.
    Bado Mtakatifu Tom ameendelea kusikitikia matokeo ya kuanza na sare katika Ligi Kuu dhidi ya Prisons, lakini amesema sasa anaelekeza nguvu zake katika mechi ijayo dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Jumatano.
    Mbelgiji huyo, alilalamikiwa wapinzani wake, Prisons kucheza soka ya kuudhi tangu mwanzo, ndiyo maana wakapata sare ya bila kufungana kwenye Uwanja wa nyumbani kwao, Sokoine mjini Mbeya.
    Hata hivyo, Saintfiet alisema amejifunza jambo na anayakubali matokeo hayo na sasa anajipanga kwa ajili ya mchezo ujao.
    “Ilikuwa mechi ngumu, Prisons walicheza soka ya kuudhi, wakipoteza muda tangu sekunde ya kwanza,”alisema kocha huyo, ambaye hiyo inakuwa sare yake ya kwanza tangu aanze kufundisha Yanga Julai mwaka huu, akiwa ameshinda mechi 11 na kufungwa moja.
    Mtakatifu Tom alisema kwamba pamoja na ugumu huo, lakini kipindi cha pili walipata nafasi za kufunga mabao, ila bahati mbaya walishindwa kuzitumia vema na hana cha kulamu kwa sababu katika soka wakati mwingine mambo huwa hivyo.
    “Kipindi cha pili tulistahili pointi tatu, Hamisi Kiiza alipiga mashuti matatu mazuri na Simon Msuva pia moja, lakini kipa wa Prisons akaokoa vizuri sana, hatukucheza kwa ubora wetu, lakini siwezi kuwalaumu wachezaji wangu, walipambana, nimesononeka sana,”alisema Mtakatifu alipozungumza na BIN ZUBEIRY kwa simu kutoka Mbeya jana.
    Yanga Jumamosi ilianza vibaya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, huku wapinzani wao wakubwa katika mbio za taji, Simba na Azam wakiibuka na ushindi.  
    Simba iliichapa African Lyon mabao 3-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wafungaji Emanuel Okwi, Nassor Masoud ‘Chollo’ na Daniel Akuffo, wakati Azam iliichapa Kagera Sugar 1-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba, mfungaji Abdulhalim Humud.
    Katika mechi nyingine za ligi hiyo, kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga, bao pekee la kiungo Mkenya, Jerry Santo dakika ya 41 liliipa Coastal Union ushindi wa 1-0 dhidi ya Mgambo FC.
    Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, wenyeji Polisi wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Mtibwa Sugar ya Turiani, Manungu.
    Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, Toto Africans imelazimishwa sare ya 1-1 na JKT Oljoro, wakati Uwanja wa Chamazi, Mbagala, JKT Ruvu imeifunga Ruvu Shooting mabao 2-1.

    REKODI YA SAINTFIET YANGA
    1.              Yanga Vs JKT Ruvu (Kirafiki)                     2-0
    2.              Yanga Vs Atletico (Burundi, Kagame)     0-2
    3.              Yanga Vs Waw Salam (Sudan, Kagame) 7-1
    4.              Yanga Vs APR (Rwanda, Kagame)           2-0
    5.              Yanga Vs Mafunzo (Z’bar, Kagame)       1-1 (5-3penalti)
    6.              Yanga Vs APR (Rwanda, Kagame)           1-0
    7.              Yanga Vs Azam              (Kagame)            2-0
    8.              Yanga Vs African Lyon (Kirafiki)               4-0
    9.              Yanga Vs Rayon (Kirafiki, Rwanda)         2-0
    10.             Yanga Vs Polisi (Kirafiiki, Rwanda)          2-1
    11.             Yanga Vs Coastal Union    (Kirafiki)         2-1
    12.             Yanga Vs Moro United      (Kirafiki)         4-0
    13.             Yanga Vs Prisons                 (Ligi Kuu)       0-0 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NIYONZIMA HATARINI KUWAKOSA MTIBWA SUGAR KESHOKUTWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top