• HABARI MPYA

    Friday, September 21, 2012

    PIGO AZAM, HUMU AINGIA WADI YA WAGONGWA CHAMAZI

    Humud katika mechi ya Ngao na Simba, akipambana kutafuta bao dhidi ya beki Amir Maftah na kipa wake, Juma Kaseja

    Na Prince Akbar
    PIGO Azam FC. Kiungo ambaye yuko juu ile mbaya kwa sasa kisoka, Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ amerejea na maumivu kutoka Kanda ya Ziwa baada ya kuumia kwenye mechi ya juzi dhidi ya Toto African, Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulioisha kwa sare ya 2-2.
    Humud anaingia kwenye ‘wadi ya wagonjwa’ Chamazi, ambako tayari wamo viungo Salum Abubakar ‘Sure Boy Jr.’, Hamisi Mcha ‘Vialli’ na mshambuliaji Ibrahim Jeba, ingawa yeye tatizo lake linaweza kuwa la muda mfupi.
    Humud alifunga katika kila mechi kwenye mbili za Ligi Kuu ilizocheza Azam, dhidi ya Kagera Sugar, Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba bao pekee la ushindi na jana katika sare ya 2-2 na Toto alifunga moja na lingine Kipre Herman Tchetche.
    Azam FC inatarajiwa kuwa na mchezo mgumu Jumamosi kwenye Uwanja wa Chamazi, dhidi ya Mtibwa Sugar, ambayo nayo ineonekana kuwa tishio msimu huu.
    Mtibwa iliyoifunga Yanga 3-0 juzi, ina pointi sawa na Azam, nne kila moja na mechi ya Jumamosi itakuwa kali kwa sababu kila timu itahitaji ushindi kumuacha mwenzake.
    Ikumbukwe msimu uliopita wa Ligi Kuu, Azam na Mtibwa zilicheza mechi tatu baada ya mbili, kutokana na mechi moja kuvunjika Chamazi na kurudiwa katika Uwanja wa Taifa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PIGO AZAM, HUMU AINGIA WADI YA WAGONGWA CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top