• HABARI MPYA

    Friday, September 21, 2012

    OCHIENG ACHUNGULIA MLANGO WA KUTOKEA SIMBA SC

    Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia han Poppe akimkabidhi jezi Paschal Ochieng baada ya kukamilisha usajili. Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu'.

    Na Mahmoud Zubeiry
    BEKI Mkenya Paschal Ochieng ana kazi kubwa ya kufanya kujiepusha katika hatari ya kutupiwa virago Simba SC Desemba mwaka huu, kwani sasa anakabiliwa na wakati mgumu katika klabu hiyo.
    Ochieng aliyesajiliwa kutoka AFC Leopard ya Kenya, kwa pamoja na beki kutoka Mali, Komabil Keita waliondolewa kwenye kikosi cha kwanza cha Simba SC na Kocha Mserbia, Milovan Cirkovick ili warekebishe makosa yao taratibu.
    Inaonekana kama Keita anaanza kuiva na kukaribia kurejea kwenye kikosi cha kwanza, baada ya jana kupangwa katika kikosi kilichocheza mechi ya kirafiki na Moro United Uwanja wa Kinesi.
    Katika mchezo huo, bao pekee la mfungaji bora wa mashindano ya Kombe la BancABC, Christopher Edward dakika ya 43 liliipa ‘Simba Rizevu’ ushindi wa 1-0.
    Katika mchezo huo, Edward ambaye utampenda mazoezini akipangwa timu moja na Mrisho Ngassa jinsi wanavyoelewana ‘utafikiri walizaliwa pamoja’ angeweza kufunga hata mabao matatu kama angetumia vema nafasi zote alizopata.
    Kikosi cha Simba jana kilikuwa; Albert Mweta/Hamadi Waziri, Haruna Shamte/Ramadhan Singano ‘Messi’, Komabil Keita, Paul Ngalema, Jonas Mkude, Kiggi Makassy, Haroun Othman, Christopher Edward, Salim Kinje/Omar Seseme na Felix Sunzu.
    Awali ya hapo, Simba ilicheza mechi ya Ligi Kuu juzi na kuifunga JKT Ruvu mabao 2-0, wafungaji viungo Amri Kiemba na Haruna Moshi ‘Boban’. Katika mchezo huo wa pili mfululizo Simba kushinda baada ya awali kuifunga African Lyon 3-0, kikosi kilikuwa; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Shomary Kapombe, Juma Nyosso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi ‘Boban’, Daniel Akuffo/Ramadhan Chombo, Mrisho Ngassa/Abdallah Juma na Emanuel Okwi. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: OCHIENG ACHUNGULIA MLANGO WA KUTOKEA SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top