![]() |
Edo Boy |
Na Mahmoud Zubeiry
SIMBA SC ni
baab kubwa- kama hupendi jinyonge. Achana na wanaume wale waliocheza jana na
kuitandika JKT Ruvu mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, hata wale ambao hawakucheza mechi ya jana
ni wa ushindi pia.
Habari ndiyo
hiyo, leo wachezaji ambao hawakushiriki mechi ya jana wamecheza mechi ya
kirafiki na timu iliyokuwa Ligi Kuu msimu uliopita tu, Moro United kwenye
Uwanja wa Kinesi na kutoa adhabu.
Mfungaji bora
wa mashindano ya Kombe la BancABC, Christopher Edward ndiye alikuwa ‘sterling’
wa kikosi cha wachezaji wa akiba cha Simba leo Kinesi, kwa kufunga bao pekee
dakika ya 43.
Katika mchezo
huo, Edward ambaye utampenda mazoezini akipangwa timu moja na Mrisho Ngassa
jinsi wanavyoelewana ‘utafikiri walizaliwa pamoja’ angeweza kufunga hata mabao matatu
kama angetumia vema nafasi zote alizopata.
Kikosi cha
Simba leo kilikuwa; Albert Mweta/Hamadi Waziri, Haruna Shamte/Ramadhan Singano ‘Messi’,
Komabil Keita, Paul Ngalema, Jonas Mkude, Kiggi Makassy, Haroun Othman, Christopher
Edward, Salim Kinje/Omar Seseme na Felix Sunzu.
0 comments:
Post a Comment