• HABARI MPYA

    Thursday, September 20, 2012

    YANGA WAINGIA KAMBINI JANGWANI

    Mbuyu Twite akishuka kwenye basi jana Uwanja wa Jamhuri

    Na Mahmoud Zubeiry
    YANGA SC wamekumbuka kitu kinaitwa kambi, baada ya kuanza vibaya katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na hivi unaposoma habari hii, wachezaji wote wa timu hiyo, kasoro majeruhi wa muda mrefu, Salum Telela leo wamewaachia vitanda wake wazo peke yao na watalala makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani.
    Hatua hiyo inafuatia kuambulia pointi moja katika mechi mbili za Ligi Kuu, ikitoa sare na Prisons 0-0 mjini Mbeya Jumamosi na kufungwa 3-0 na Mtibwa Sugar mjini Morogoro jana.
    Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, wachezaji 30 wameingia kambini leo katika hosteli ya klabu, Jangwani kujiandaa na mchezo wa Jumamosi dhidi ya JKT Ruvu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Hafidh amewataja wachezaji hao kuwa ni  Nizar Khalfan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Shamte Ally Kilalile, Said Rashid Bahanuzi, Haruna Niyonzima Fadhili, Didier Kavumbagu Fortine, Juma Seif Dion ‘Kijiko’, Nadir Haroub Ally ‘Cannavaro’, Nurdin Bakari Hamad, Said Mohamed, Rashid Omary Gumbo, Juma Jaffar Abdul, Omega Sunday Seme na Kevin Yondan Patrick.
    Wengine ni Jerson John Tegete, Idrisa Rashid Abdallah, Godfrey Taita Magina, Oscar Joshua Nkulula, David Charles Luhende, Ibrahim Job Isaac, Ladislaus Mbogo Mahendeka, Ally Mustafa Mtinge ‘Barthez’, Shadrack Joel Nsajigwa, Hamisi Friday Kiiza, Yaw Koffi Berko, Stephano Asangalwisye Mwasyika, Mbuyu Twite Banza, Simon Msuva, Frank Domayo na Issa Ngao.
    Wakati Yanga wanakumbuka kambi baada ya kupoteza pointi tano katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu, tangu wamerejea kutoka Arusha wiki wiki mbili zilizopita, wapinzani wao wa jadi, Simba SC wamekuwa kambini hoteli ya Sapphire, Kariakoo, Dar es Salaam.
    Kuanza vibaya kwa Yanga katika Ligi Kuu kumeibua maswali na maoni mengi, kocha akisema wachezaji wamevimba vichwa na hawajitumi tena, jambo ambalo limeungwa mkono na uongozi ambao sasa unawaweka chini ya uangalizi maalum wachezaji hao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA WAINGIA KAMBINI JANGWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top