![]() |
| Yanga SC |
Na Princess Asia
KOCHA Mkuu
wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet anatarajiwa kuiongoza timu yake katika mazoezi
ya kwanza kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya leo, ili kuuonja klabla ya mechi
ya kesho ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Prisons.
“Baada ya
safari ya saa 14 na dakika 30, tumefika Mbeya salama,”alisema Mtakatifu Tom
alipozungumza kwa simu na BIN ZUBEIRY jana, saa 4:00 usiku.
Tayari Mtakatifu
Tom amesema kwamba mechi hiyo itakuwa ngumu kwa sababu anaamini wapinzani wao
watakamia na watasaidiwa na kucheza nyumbani.
Lakini pia,
Saintfiet alisema Prisons haina presha ya kufungwa na Yanga kwa sababu ni timu
kubwa, hivyo watacheza kwa utulivu, wakipata sare ni safi, wakifungwa hakuna
tatizo na wakishinda kwao itakuwa ‘sikukuu’.
Kwa sababu
hizo, Mtaalamu huyo wa Kibelgiji anaamini mechi hiyo itakuwa ngumu kwao na timu
yake inaondoka leo Dar es Salaam kwenda Mbeya ikilijua hilo.
Mtakatifu
Tom ametaua wachezaji 22 kwa ajili ya mechi hiyo na amesema ameteua wachezaji
hao kulingana na mazingira ya mechi yenyewe na kwamba wachezaji wengine wote
waliobaki ni wazuri pia.
Aliwataja
wachezaji aliowateua kuwa ni makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki
Shadrack Nsajigwa, Juma abdul, Godfrey Taita, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, David Luhende, Oscar
Joshua na Stefano Mwasyika.
Aliwataja
viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Rashid Gumbo, Nizar
khalfan, Shamte Ally na Simon Msuva, wakati washambuliaji ni Jerry Tegete,
Didier Kavumbangu, Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza.
Aliwataja
wachezaji wa kikosi cha kwanza ambao hawatasafiri kwa ajili ya mechi hiyo kuwa
ni kipa Said Mohamed, Ladislaus Mbogo, Job Ibrahim, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela,
Omega Seme, Nurdin Bakari, Idrisa Assega na Issa Ngao wa Yanga B, ambaye
anakomazwa kikosi cha kwanza.
Jumamosi
Yanga ilicheza mechi ya mwisho ya kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu
na kushinda mabao 4-0 dhidi ya Moro united, Mrundi Didier Kavumbangu akifunga
mawili, mengine beki Juma Abdul na kiungo Shamte Ally.
“Kavumbangu
aliwahi kufunga pia tulipocheza na Sinza Stars, ninafurahia hilo, ni muhimu kwa
klabu kubwa, lakini pia wachezaji wengine wanaweza kufunga, Stefano Mwasyika,
Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul…tumecheza mechi 14 kabla ya ligi, zikiwemo
dhidi ya Sinza Stars na Kijitonyama Stars, tumefunga mabao 42 na tumefungwa
sita tu,”alisema Mtakatifu Tom.
Saintfiet alitaka
mechi moja dhidi ya timu inayocheza kama wapinzani wao wa kwanza katika Ligi
Kuu, Prisons na pia katika Uwanja mbaya kama ambao atachezea mechi ya kwanza ya
ligi hiyo, Sokoine mjini Mbeya na ndiyo maana timu hiyo ikacheza na Moro United
juzi kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kijitonyama.
Saintfiet
ameridhika na kiwango cha timu na sasa anasema timu iko tayari kwa Ligi Kuu,
akianza na Prisons iliyorejea Ligi Kuu msimu huu kwenye Uwanja wa Sokoine, Septemba
15.
Hiyo ilikuwa mechi ya 11, Saintfiet anashinda
Yanga katika mechi 12 tangu ajiunge nayo miezi miwili iliyopita, mbali ya ziwe
za mazoezini dhidi ya Sinza Stars na Kijitonyama Stars.
Ndani ya mechi hizo kuna mechi sita za
Klabu Bingwa ya soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, ambalo
aliiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa tano wa michuano hiyo, ikipoteza mechi moja
tu ya kwanza dhidi ya Atletico ya Burundi, kwa kufungwa 2-0, mabao yote ya
Kavumbangu, ambaye baadaye ikamsajili.



.png)
0 comments:
Post a Comment