• HABARI MPYA

    Friday, March 15, 2013

    ADEBAYOR AIPELEKA ROBO FAINALI SPURS ULAYA


    BAO la Emmanuel Adebayor dhidi ya wabaguzi wa rangi, Inter Milan limeiwezesha Spurs kutinga Robo Fainali ya Europa League usiku wa jana.
    Lilikuwa bao liliwajibu mashabiki wa Inter ambao mwishoni mwa kipindi cha kwanza walimuitia ndizi jukwaani Adebayor wakimfananisha na nyani.
    Matokeo ya jumla baada ya mechi zote mbili yanakuwa 4-4, lakini kwa bao la Adebayor jana Spurs ikilala 4-1 San Siro, imefuzu kwa faida ya bao la ugenini, kwani yenyewe awali ilishinda 3-0 London.

    VIKOSI...

    Inter Milan: S Handanovic, Zanetti, Chivu, Juan, Jonathan/Andrea Ranocchia dk108, Guarin/Alvarez dk71, Cambiasso, Gargano, Kovacic/Benassi dk79, Palacio, Cassano
    Benchi: Belec, Pasa, Belloni, Colombi
    Kadi ya njano: Juan
    Wafungaji wa mabao: Cassano dk20, Palacio dk52, Gallas dk75 (kujifunga), Alvarez dk110

    Tottenham: Friedel, Vertonghen, Gallas, Naughton/Caulker dk104, Walker, Parker, Sigurdsson, Livermore/Lennon dk70, Adebayor, Defoe/Holtby dk56, Dembele
    Benchi: Lloris, Assou-Ekotto, Huddlestone, Carroll
    Booked: Friedel, Livermore, Walker, Holtby, Adebayor
    Mfungaji wa bao: Adebayor dk96
    Refa: Ivan Bebek (Croatia)
    Mahudhurio: 18,241

    Just about: Emmanuel Adebayor scores Tottenham's first goal in extra time
    Emmanuel Adebayor akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia bao Tottenham katika dakika za nyongeza

    ZILIZOINGIA ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE 

    Tottenham, Chelsea, Newcastle, Rubin Kazan,Fenerbahce, Lazio, FC Basle, Benfica
    Suprs jana ilicheza bila nyota wake Gareth Bale, ambaye alikuwa anatumikia aadhabu ya kadi tatu za njano kuanzia mechi ya kwanza dhidi ya Inter Milan, Aaron Lennon aliyechukua nafasi yake alifanya kazi nzuri ya kupendeza
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ADEBAYOR AIPELEKA ROBO FAINALI SPURS ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top