• HABARI MPYA

    Friday, March 15, 2013

    ENGLAND WAFURAHIA KUTOKUTANISHWA NA LAZIO ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE


    TIMU zote tatu za England zimepangwa tofauti katika Robo Fainali ya Ligi Europa.
    Baada ya kufuzu ndani ya dakika 120 dhidi ya Inter Milan, Tottenham imepangwa kumenyana na FC Basel, wakati Chelsea itamenyana na Rubin Kazan na Newcastle itakwana na Benfica.
    Kila timu inafurahia kutokutanishwa na Lazio, ambao wanafikiriwa kuwa wagumu, lakini Chelsea itatakiwa kusafiri hadi Urusi kucheza mechi yao ya ugenini.
    Mechi za kwanza itachezwa Alhamisi ya Aprili 4, wakati marudiano zitachezwa wiki moja baadaye Aprili 11.
    Crucial: Emmanuel Adebayor slides in to score the vital away goal against Inter Milan
    Emmanuel Adebayor akiteleza kufunga bao muhimu dhidi ya Inter Milan

    RATIBA ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE...

    Chelsea v Rubin Kazan
    Tottenham v Basel
    Fenerbahce v Lazio
    Benfica v Newcastle
    Mechi za kwanza Aprili 4 na marudiano Aprili 11

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ENGLAND WAFURAHIA KUTOKUTANISHWA NA LAZIO ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top