Nahodha wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na klabu ya Simba, Juma Kaseja akiwa na mdogo wake Abdulrahman, baada ya sala ya Ijumaa, waliosali katika msikiti wa Kipata, Kariakoo, Dar es Salaam. Kaseja ni mfano wa kuigwa wa wachezaji waumini wa dini ya kiislamu Tanzania, kutokana na kufanya ibada inavyotakiwa, kama kusali sala tano, kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani.