• HABARI MPYA

    Friday, March 15, 2013

    ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA; REAL NA AKINA DROGBA, BARCA NA AKINA BECKHAM ILA KAZI IPO JUVE NA BAYERN


    DROO YA ROBO FAINALI ULAYA...

    Malaga v Borussia Dortmund
    Real Madrid v Galatasaray
    PSG v Barcelona
    Bayern Munich v Juventus
    (Mechi zitachezwa Aprili 2 na 3 na marudiano Aprili 9 na 10.
    IMETOKA DAILY MAIL UK
    KIUNGO David Beckham na timu yake PSG watamenyana na Lionel Messi na Barcelona katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
    Wakati Zlatan Ibrahimovic ataikosa mechi ya kwanza kutokana na kutumikia adhabu, Barcelona watakuwa na matumaini ya kupata matokeo mazuri kwenye mchezo wa marudiano nyumbani  Nou Camp.
    Katika droo iliyopangwa mjini Nyon, timu mbili zinazopewa nafasi kubwa Real Madrid na Barcelona, zinaonekana kupangiwa timu vibonde, lakini Jose Mourinho atatumai faraja kukutana tena na mshambuliaji wake wa zamani Didier Drogba.
    Borussia Dortmund itamenyana na Malaga na vigogo wengine wawili Ulaya, Bayern Munich na Juventus watapambana wenyewe kwa wenyewe Uwanja wa Allianz.

    DROO YA ROBO FAINALI EUROPA LEAGUE NAYO HII HAPA...

    Mechi ya kwanza - April 4 
    Chelsea v Rubin Kazan
    Tottenham v Basle
    Fenerbahce v Lazio
    Benfica v Newcastle
    Mechi ya marudiano - April 11
    Rubin Kazan v Chelsea
    Basle v Tottenham
    Lazio v Fenerbahce
    Newcastle v Benfica
    Hello Leo: David Beckham and PSG will face Messi's Barcelona

    Karibu Leo: David Beckham na PSG watamenyana na Messi na Barcelona yake
    Jose Mourinho
    Didier Drogba
    Marafiki wanakutana: Kocha wa zamani Chelsea, Jose Mourinho (kushoto) atapambana na mshambuliaji wake wa zamani, Didier Drogba

    Mechi za kwanza za Robo Fainali zitachezwa Aprili 2 na 3 na marudiano zitakuwa Aprili 9 na 10, wakati droo ya Nusu Fainali itapangwa Aprili 12.
    The biggest prize: The eight teams will battle it out for the European Cup
    Taji kubwa: Timu nane zitamenyana sasa kuwania ndoo hii ya thamani kubwa Ulaya
    Away tie: Borussia Dortmund will travel to Malaga in the first leg
    Wanaanzia ugenini: Borussia Dortmund wataifuata Malaga katika mechi ya kwanza
    To Istanbul: Cristiano Ronaldo will travel to meet Didier Drogba and Galatasaray
    Safari Istanbul: Cristiano Ronaldo atasafiri kumfuata Didier Drogba na Galatasaray yake
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA; REAL NA AKINA DROGBA, BARCA NA AKINA BECKHAM ILA KAZI IPO JUVE NA BAYERN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top