• HABARI MPYA

    Saturday, March 09, 2013

    MAN UNITED WAWASAIDIA WAPINZANI WA MAN CITY KOMBE LA FA


    KLABU ya Barnsley imepewa msaada na kocha wa Manchester United, Sir Alex Ferguson katika jitihada zao za kuing'oa Manchester City kwenye raundi ya sita ya Kombe la FA leo Jumamosi Uwanja wa Etihad.
    Baada ya sare ya 1-1 nyumbani Burnley usiku wa Jumanne, kocha wa Barnsley David Flitcroft aliwapangia wachezaji wake hoteli na kuandaa mazingira ya kufanya mazoezi maeneo ya Manchester katika siku tatu zilizofuata.
    Habari njema kwao ni kwamba, Man United ikawakubali kuwafungulia ya Uwanja wao wa mazoezi, Carrington ili klabu hiyo ya Daraja la Kwanza ijifue hapo.
    Kumbuka, Man City waliwapa Uwanja wa mazoezi Real Madrid walipokwenda kumenyana na United katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki hii na sasa Mashetani Wekundu wanalipa kisasi.
    Upset: David Flitcroft's Barnsley trained at United's training ground in a bid to produce a Cup shock over City
    Kocha David Flitcroft wa Barnsley akiwa mazoezini kwenye Uwanja wa Man United kujiandaa kuing'oa City
    Helping hand: Sir Alex Ferguson opened to doors of Carrington to the lower league side on Thursday
    Sir Alex Ferguson amewafungulia milango wapinzani wa City Carrington tangu juzi
    Man City v Barnsley
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAN UNITED WAWASAIDIA WAPINZANI WA MAN CITY KOMBE LA FA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top