• HABARI MPYA

    Saturday, March 09, 2013

    MASHABIKI WA AL AHLY WACHOMA MOTO OFISI ZA SHIRIKISHO BAADA YA KORTI KUIDHINISHA HUKUMU YA KIFO KWA WENZAO LEO


    MASHABIKI wa klabu ya Al-Ahly ya Cairo, wamevamia ofisi za Shirikisho la Soka Misri makao makuu na kuzichoma moto kwa hasira za wenzao kuhukumiwa kifo kutokana na vurugu za mwaka jana kwenye Uwanja wa Port Said. 
    Mapema leo, Korti ya Cairo imethibitisha hukumu ya kifo waliyopewa mashabiki wa soka 21 kutokana na kuhusika na vurugu hizo, ambazo zilisababisha vifo vya watu 74 na wengine 1,000 kujeruhiwa.
    Moto pia ulifika hadi kwenye kituo cha Polisi jirani, lakini haijajulikana kwa uhakika kama ni mashabiki wa Al-Ahly waliohusika na tukio hilo. 
    Supporters of Al-Ahly football club react after the verdict in the Port Said stadium riot trial was announced today
    Mashabiki wa Al-Ahly wakihamaki baada ya hukumu ya  kifo kwa wenzao kuidhinishwa leo kutokana na vurugu za Uwanja wa Port Said mwaka jana
    In Cairo, Al-Ahly fans greeted the verdicts but violence soon erupted
    Ndani ya Cairo, mashabiki wa Al-Ahly wakichoma moto ofisi za shirikisho
    A man reacts to the court's decision in Port Said today. Most of those sentenced to death are fans of the city's Al Masry club
    Jamaa akilalamikia uamuzi wa korti leo kuhusu tukio la vurguu kwenye Uwanja wa Port Said mwaka jana. Wengi wa waliohukumiwa kifo ni mashabiki wa Al Masry
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MASHABIKI WA AL AHLY WACHOMA MOTO OFISI ZA SHIRIKISHO BAADA YA KORTI KUIDHINISHA HUKUMU YA KIFO KWA WENZAO LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top