• HABARI MPYA

    Friday, June 14, 2013

    ABDALLAH MSAMBA ALIVYOPUMZISHWA KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE MAGOMENI MAKUTI DAR ES SALAAM LEO

    IMEWEKWA JUNI 14, 2013 SAA 11:00 JIONI
    MWANASOKA wa zamani wa Tanzania, Abdallah Msamba amezikwa mchana wa leo makaburi ya Magomeni Makuti, Dar es Salaam katika mazishi yaliyohudhuriwa na mamia ya wachezaji mbalimbali, wengi wakiwa wastaafu na haswa aliocheza nao enzi zake.
    Shrikisho la Soka Tanzania (TFF) liliwakilishwa na Mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji, Ahmed Mgoyi, wakati sehemu kubwa ya walioshiriki walikuwa ni wachezaji tu.  
    TFF imesema imepokea  kwa masikitiko taarifa za kifo cha mchezaji huyo wa zamani wa timu za Pan Africans, Simba na Taifa Stars, Abdallah Msamba kilichotokea juzi usiku (Juni 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
    TFF imesema msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Msamba akiwa mchezaji, na baadaye kocha wa timu kadhaa alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea na kufundisha ikiwemo Villa Squad, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
    Imesema  inatoa pole kwa familia ya marehemu Msamba, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kinondoni (KIFA) na klabu ya Villa Squad na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
    Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu Abdallah Msamba

    Wakiwa kwenye kaburi la marehemu baada ya mazishi. Hapa mkakati ni kulijengea.

    Boniface Pawasa kushoto akizungumza jambo baada ya mazishi

    Ally Mayay akizungumza jambo baada ya mazishi

    Kulia Iddi Moshi na kushoto Twaha Hamidu 'Noriega'

    Mabeki wa zamani wa Simba SC, Amri Said na Adolph Kondo kushoto

    Mdau maarufu wa soka nchini na Meneja wa zamani wa Yanga SC, Hamisi Ambari kushoto akiwa na wachezaji mbalimbali

    Wachezaji mbalimbali msibani

    Wachezaji mbalimbali wa zamani msibani 

    Kocha wa Simba Jamhuri Kihwelo akizungumza baada ya mazishi. Kushoto kwake ni George Lucas na nyuma ni Iddi Selemani na John Mwansasu


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ABDALLAH MSAMBA ALIVYOPUMZISHWA KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE MAGOMENI MAKUTI DAR ES SALAAM LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top