• HABARI MPYA

    Friday, May 16, 2014

    KOZI ZA UKOCHA LESENI A, B KUFANYIKA JUNI

    Na Boniface Wambura, Darv es Salaam
    KOZI za ukocha wa mpira wa miguu kwa ajili ya leseni A na B zinazotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)  zitafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 2 mwaka huu.
    Ada kwa kozi zote ni sh. 300,000 ambapo wale watakaofanya ya A (equivalent) itaanza Julai 21-26 mwaka huu. Washiriki wa kozi hiyo ni wale wenye leseni B za ukocha za CAF.
    Kwa wale watakaoshiriki kozi ya leseni B ambao ni wale wenye leseni C watakuwa na vipindi viwili. Kipindi cha kwanza ni kuanzia Juni 2-15 mwaka huu wakati cha pili kinaanza Juni 23 mwaka huu na kumalizika Juni 28 mwaka huu.

    Wakufunzi wanaotambuliwa na CAF watakaoendesha kozi hiyo ni Sunday Kayuni na Salum Madadi kutoka Tanzania, na washiriki watajigharamia kwa kila kitu. Baadaye CAF watatuma Mkufunzi mwingine kwa ajili ya mitihani.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOZI ZA UKOCHA LESENI A, B KUFANYIKA JUNI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top