• HABARI MPYA

    Wednesday, December 05, 2012

    NGASSA, BOCCO WAMNYIMA USINGIZI UMONY


    Umony
    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MSHAMBULIAJI wa Uganda, Brian Umony amesema kwamba katika mechi mbili zilizobaki za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge atajitahidi awapiku wachezaji wa Tanzania, John Bocco na Mrisho Ngassa katika ufungaji wa mabao kwenye michuano hiyo.
    “Mimi nina mabao matatu, wao kila mmoja ana mabao matano, sijakata tamaa, nitajitahidi niwapiku, najua ni kazi ngumu, lakini nitajitahidi sana,”alisema mchezaji huyo ambaye ameonyesha nia ya kujiunga na Simba SC ya Dar es Salaam.
    Akiizungumzia mechi ya Nusu Fainali dhidi yao na Tanzania Bara kesho, Umony alisema anaamini itakuwa ngumu sana, lakini watapambana kushinda.
    “Tanzania wana timu nzuri sana, ina wazoefu ambao mimi nawajua kama Mrisho Ngassa na Juma Kaseja, kwa kweli mchezo utakuwa mgumu, itakuwa mechi nzuri sana yenye hadhi ya fainali,”alisema Umony.
    Brian amerejea nyumbani Uganda na kujiunga na Express baada ya kumaliza mkataba wake, Becamex Binh Duong F.C. ya Vietnam.
    Mwaka 2009, baada ya Simba kuzidiwa kete na SuperSport United ya Afrika Kusini kwa Umony, ikamsajili Emmanuel Okwi aliyekuwa SC Villa wakati huo.
    Umony aliichezea Supersport United hadi 2010 alipohamia University of Pretoria ya Afrika Kusini pia hadi mwaka 2011 alipohamia Portland Timbers ya Marekani kwa mkopo na mwaka huu akatua Becamex Binh Duong F.C.
    Tayari Umony amesema anaweza kujiunga na Simba wakiafikiana naye dau.

    WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
    John Bocco                    Tanzania  5
    Mrisho Ngassa               Tanzania  5
    Brian Umony                  Uganda    3
    Suleiman Ndikumana     Burundi    3 (1 penalti)
    Chris Nduwarugira         Burundi    3
    Geoffrey Kizito               Uganda    2
    Robert Ssentongo          Uganda    2
    Khamis Mcha                 Zanzibar   2
    David Ochieng               Kenya       2
    Clifton Miheso                Kenya       2
    Dadi Birori                      Rwanda    2
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NGASSA, BOCCO WAMNYIMA USINGIZI UMONY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top