• HABARI MPYA

    Wednesday, December 05, 2012

    SSENTONGO SASA AITAKA MWENYEWE SIMBA SC

    Ssentongo

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MSHAMBULIAJI wa Uganda, Robert Ssentongo amesema kwamba atakuwa tayari kujiunga na Simba SC ya Dar es Salaam, wakiafikiana naye dau.
    Ssentongo anayeng’ara katika Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, amewahi kuchezea Simba kwa muda tu katika Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, mwaka juzi mjini Kigali, Rwanda.
    Lakini baada ya michuano hiyo, akatemwa na badala yake akasajiliwa kiungo Mganda mwenzake, Patrick Ochan ambaye baada ya msimu mmoja aliuzwa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    “Mimi nipo tayari Simba wakinitaka, wao wafike bei tu, ile ni timu kubwa na ninaamini nikijiunga nayo nitapata mafanikio,”alisema.
    Ssentongo amewahi kucheza African Lyon ya Dar es Salaam na alipomaliza mkataba wake akachezea Simba kwa muda kabla ya kurejea Uganda.
    Awali Ssentongo aliwahi kuchukua fedha za Simba, lakini hakuja kujiunga nayo hadi alipokuja Lyon.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SSENTONGO SASA AITAKA MWENYEWE SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top