• HABARI MPYA

    Wednesday, December 05, 2012

    WALEVI, WAZINZI HARAMBEE STARS WAPANDISHWA NDEGE KUJA KUIVAA ZANZIBAR HEROES KESHO

    Paul Were

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    KATIKA kile kinachoonekana kuwa ni mchecheto wa mechi dhidi ya Zanzibar, Kenya imeongeza wachezaji wawili Paul Were na Kevin Omondi kwa ajili ya mechi hiyo ya Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge inayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini hapa.
    Wawili hao waliondoka jana usiku Nairobi, mara tu baada ya Harambee Stars kuvuzu Fainali, wakiifunga 1-0 kwa mbinde Malawi na tayari wapo Kampala, Uganda kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya Zanzibar Stars.
    Baada ya kuifunga 1-0 Sudan Kusini katika mchezo wa pili wa Kundi A, wachezaji hao walikwenda kujirusha kwenye klabu ya usiku na kurejea kambini na wanawake, jambo ambalo lilifanya asubuhi yake waoandishwe ndege wote kurejea Nairobi, lakini kutokana na mchecheto wa mechi ya kesho, wamerejeshwa.
    Kocha wa Harambee Stars, James Nandwa aliliomba Shirikisho la Soka Kenya (FKF) liliwarejeshe wachezaji hao kwa ajili ya Nusu Fainali.
    Kocha wa Fisa FC, Charles ‘Korea’ Omondi, ambaye amekuwa akifanya mazoezi na wachezaji hao tangu warejeshwe nyumbani, amethibitisha wamebadilika kinidhamu na wako vizuri kimchezo.
    Were na Omondi wapo kwa mkopo AFC Leopards na Gor Mahia kutoka timu inayoshiriki Ligi ya Jimbo la Nairobi, Fisa FC.
    Mchezo kati ya Zanzibar Heroes na Kenya utaanza kesho saa 10:00 jioni, ukifuatiwa na Nusu Fainali ya pili, kati ya Uganda na Tanzania Bara Kilimanjaro Stars.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: WALEVI, WAZINZI HARAMBEE STARS WAPANDISHWA NDEGE KUJA KUIVAA ZANZIBAR HEROES KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top