• HABARI MPYA

    Thursday, April 12, 2012

    MASHABIKI AFRIKA KUSINI WAMZOMEA KIPA WAO KWA KUFUNGWA BAO LA MASAFA MAREFU



    Kipa wa Pirates
    KOCHA wa Orlando Pirates, Augusto Palacios amesema kwamba mashabiki waliomzomea kipa Senzo Meyiwa Jumatatu hawana aibu.

    Meyiwa, ambaye alichukua nafasi ya Moeneeb Josephs, alizomewa kwa kufungwa bao la mbali la kiungo wa Jomo Cosmos, Siyabonga Nhlapho ingawa timu yake ilishinda 2-1 dhidi ya Ezenkosi katika mechi ya Ligi Kuu Uwanja wa Orlando.

    Kocha huyo raia wa Peru amesema aibu ni kwamba mashabiki wa Pirates wanamzomea mchezaji wao wenyewe.

    "Kitu kimoja ambacho sikukupenda kwenye mechi hiyo ilikuwa ni jinsi mashabiki walivyopmfanyia Senzo,”alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MASHABIKI AFRIKA KUSINI WAMZOMEA KIPA WAO KWA KUFUNGWA BAO LA MASAFA MAREFU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top