• HABARI MPYA

    Thursday, April 12, 2012

    TIMU YA NGASSA KUCHEZA NA CHELSEA

    Ngassa alipokuwa Marekani
    KLABU ya Chelsea itacheza na nyota wa Ligi Kuu ya soka ya Marekani, MLS All-Stars huko Philadelphia, Julai 25, mwaka huu, ikiwa sehemu ya ziara klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England nchini Marekani.
    All-Star ya MLS ilimenyana na mabingwa wa England, Manchester United mara mbili miaka miwili iliyop-ita. Chelsea ilicheza na All-Stars hiyo mwaka 2006.
    Chelsea itacheza mechi nyingine na Seattle Sounders Julai 18, mwaka huu.
    Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Poland, Peter Nowak atachezea MLS All-Stars kwenye Uwanja wa PPL Park – nyumbani kwa timu ya Philadelphia Union, ambayo hivi karibuni ilimtema kiungo Mtanzania, Nizar Khalfan.
    Mwaka jana, mshambuliaji wa Tanzania Mrisho Ngassa alipewa katika 10 kuichezea Seattle Sounders mechi ya kirafiki dhidi ya Manchester United, wakati Nizar akiwa bado Vancouver Whitecaps aliichezea katika mechi na Manchester City.
    Wakati Nizar alihamia Philadelhpia Whitecaps iliposhuka, Ngassa hakufuzu majaribio na sasa yupo Azam FC.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TIMU YA NGASSA KUCHEZA NA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top