![]() |
Nizar enzi zake Marekani |
BONANZA la Southern Zone All
Stars linalotarajiwa kufanyika Mei mwaka huu na kushirikisha nyota mbalimbali
wa soka na muziki wa kizazi kipya kama Juma Nature, Profesa Jay na Dullayo,
Nazir Khalifani na Mohamed Hussein ‘Mmachinga’
limeongeza mkakati mwingine wa kutafuta chipukizi wa muziki wa kizazi
kipya.
Akizungumza na bongostaz,
Mratibu wa bonanza hilo Mussa Chimae, amesema lengo lilikuwa kusaidia watoto
wenye ulemavu wa akili kwa ajili ya kushiriki michezo ya Olimpiki kwa walemavu,
lakini wameamua kuongeza jambo jingine.
“Tulilenga kusaidia watoto wenye
ulemavu wa akili, ambao wanatarajiwa kushiriki michezo ya Olimpiki kwa upande
wa walemavu, lakini tumeona tuongeze na jambo jingine ambapo tutatafuta vijana
wenye vipaji vya kuimba muziki,” alisema Chimae.
Chimae alisema bonanza hilo
litakalowahusisha wasanii na wachezaji mbalimbali kutoka mikoa ya Kusini
litafanyika kwa mara ya kwanza katika Mkoa wa Mtwara kwenye Uwanja wa Nangwanda
Sijaona.
“Kwa kuwa ndio tunaanza kufanya
bonanza hili kwa mara ya kwana tutafanya kwenye Mkoa wa Mtwara tu, lakini
tukiona linamafanikio tutafanya na mikia mingine ya kusini,” aliongeza Chimae.
Moja ya mambo yatakayofanyika
kwenye bonanza hilo ni pamoja na burudani na mchezo wa soka kati ya maveterani
wa Mkoa huo wa Mtwara na wasanii na wachezaji wa kutoka mikoa hiyo ya kusini.
Pamoja na akina Juma Nature na
Profesa Jay, wengine ni Z Anto, Jafaray, KR Mullah, Kaka Man, D Knob, huku
upande wa wacheji ukiwa na akina Aliphonce Amlima, Mmachina, Nizar na Salvatory
Ibrahim.
Nizar Khalfan ametemwa na klabu
ya Philadelphia Union ya Ligi Kuu ya Marekani mwezi uliopita na sasa hana timu.
Alitemwa na klabu hiyo miezi
mitatu tu tangu achukuliwe baada ya kufuzu majaribio.
Nizar alikwenda kufanya
majaribio Union, baada ya kutemwa na Vancouver, Novemba 23, mwaka jana.
Nizar aliyezaliwa Juni 21, mwaka
1988 mjini Mtwara, alijiunga na Vancouver Whitecaps FC ya Canada Agosti 22,
mwaka 2009 akitokea Moro United ya Ligi Kuu ya Bara na akacheza mechi tisa
msimu wa kwanza wa 2009 na kuongezewa mkataba wa kuichezea timu hiyo msimu
uliofuata wa 2010.
Alifunga bao lake la kwanza
Whitecaps Juni 12, mwaka 2010 katika mechi dhidi ya Austin Aztex na
haikushangaza Februari 9, mwaka jana aliposaini mkataba mpya wa mwaka mmoja
baada ya timu hiyo kupanda Ligi Kuu ya Marekani, maarufu kama Major League
Soccer.
Hata hivyo, baada ya msimu huo
timu yake ikirejea Daraja la kwanza, Niazar akatemwa na kwenda Philadelphia
Union, ambako miezi mitatu baadaye ametemwa nako.
Juhudi za kumpata Nizar
kuzungumzia mustakabali wake zinaendelea.
Kabla ya Moro United, Nizar
aliyeibukia kwenye timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti
Boys mwaka 2004, alichezea
Mtibwa Sugar FC, na baadaye
akanunuliwa na Al Tadamon ya Ligi Kuu ya Kuwait msimu wa 2007-2008.
Januari 2008 aliondoka Al
Tadamon na kusaini mkataba na Tadamon Sour ya Lebanon, ambako alipomaliza
mkataba wake akarejea Tanzania kuchezea Moro United.
0 comments:
Post a Comment