• HABARI MPYA

    Thursday, April 12, 2012

    BERRY BLACK KUTAMBULISHA MPYA BILLZ

    Berry Black akipagawisha jukwaani
    NYOTA wa muziki wa kizazi kipya Mbaraka Abdallah anatarajia kutambulisha wimbo wake mpya uitwao Nyumbani Sio Safi, Jumapili kwenye Ukumbi wa Club Billicanas.
    Berry amesema katika onyesho hilo maalumu kwa ajili ya utambulisho wa wimbo wake, ataambatana na msanii mwenzake Isihaq Salehe ‘Easy Man’, anayeng’ara na kibao cha Kasoro Wewe.
    “Katika onyesho hilo la Jumapili nitatambulisha wimbo wangu huo lakini pia nitakuwa na nyingine kibao za kuwapagawisha mashabiki wangu, nikisindikizwa na swahiba wangu Easy Man,” alsiema Berry Black.
    Berry Black, aliwa kutamba na kibao cha Nataka Kuwa na Wewe, katoka katika Kundi la 2 Berry akiwa na Berry White.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BERRY BLACK KUTAMBULISHA MPYA BILLZ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top