KLABU ya Hull City ya England, imemfukuza kocha wake Nick Barmby baada ya kipindi kisichofika miezi sita ya kuwa kazini
The Tigers wamethibitisha kwamba Barmby amesimamishwa wiki iliyopita, baada ya kufichua siri za klabu kuwa na hali mbaya kifedha.
Barmby amesema katika taarifa iliyotolewa kwa niaba yake na Chama cha Makocha wa Ligi Kuu, kwamba atakata rufaa kupinga uamuzi huo.