MSHAMBULIAJI wa Simba, Emmanuel Okwi,
amesema kama angepewa jukumu la kufanya usajili kwenye kikosi hicho, angeongeza
wachezaji wawili wapya, mmoja kwenye nafasi ya beki na mwingine kiungo.
Kwa mujibu wa gazeti la Mwanaspoti la leo, Okwi ndiye alikuwa nyota wa mchezo dhidi ya
Al-Ahly Shandy ya Sudan uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
juzi Jumapili na Simba kushinda mabao 3-0.
"Naamini kwa sasa tatizo kwenye kikosi
cha Simba lipo kwenye nafasi ya beki wa kati na kiungo," alisema Okwi
mwenye mabao 10 kwenye Ligi Kuu Bara sawa na Kenneth Asamoah wa Yanga na Nsa
Job wa Villa Squad.
Alifafanua kuwa nafasi ya beki wa kati
imekuwa ikiyumba pale inapotokea mmojawapo ameumia ama kutumikia adhabu ya kadi
nyekundu.
"Mwalimu hulazimika kumtoa Kapombe
(Shomari) beki wa kulia na kumrudisha kuziba nafasi hiyo kama ulivyoona kwenye
mchezo wa leo (juzi Jumapili)," alisema raia huyo wa Uganda.
Alisema kwa sasa kikosi hicho kinahitaji
kiungo mkabaji kama alivyokuwa Mkenya Jerry Santo.
Alisema: "Hatuna kiungo ambaye anaweza
kucheza kama alivyokuwa Santo (Jerry)."
Simba ilimrudisha beki wa kati wa Uganda,
Derrick Walulya, ambaye ameshindwa kuonyesha makali yake kwenye kikosi hicho na
mara nyingine amekosa hata namba ya kupumzika benchi
|
Will the launch of the Australian Championship help revive the embattled
A-League? Or bury it?
-
The Australian Championship launched on Friday night at Lakeside Stadium
when South Melbourne lined up against Sydney Olympic FC - and a passionate
crowd o...
24 minutes ago
0 comments:
Post a Comment