• HABARI MPYA

    Saturday, May 05, 2012

    TORRES ATAFANYA MAKUBWA, MIMI NAMALIZA KAZI LEO- RAMIRES


    FA Cup: Ramires, Tottenham v Chelsea
    Getty
    KIUNGO wa Chelsea, Ramires amesema kwamba kurejea kwa makali ya kufunga mabao kwa Fernando Torres ni moja kati ya mambo mazuri juu ya klabu hiyo kwa sasa.
    Mspanyola huyo alipiga hat trick Jumapili katika ushindi wa 6-1 dhidi ya QPR kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na mchezaji mwenzake wa Kibrazil ameelezea furaha yake juu ya kuzinduka kwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool.
    “Kitu kizuri kuhusu Chelsea? Kujiamini kwetu kumeongezeka na tuna Fernando Torres anayefunga tena," Ramires alisema. “Sasa tunaweza kumfunga yeyote na tumeonyesha hilo Camp Nou [katika fainali ya Ligi ya Mabingwa kuifunga Barcelona].”
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ataikosa fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa sababu ya kutumikia adhabu ya kazi na amesema kwamba mechi ya fainali ya Kombe la FA leo dhidi ya Liverpool itadhihirisha makali yake.
    “Kwangu, ni mechi ya msimu, kwa sababu sitacheaza fainali ya Ligi ya Mabingwa mjini Munich na ninataka kushinda taji msimu huu," alisema. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TORRES ATAFANYA MAKUBWA, MIMI NAMALIZA KAZI LEO- RAMIRES Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top