• HABARI MPYA

    Monday, May 07, 2012

    POLISI DOM, VILLA, MORO ZASHUKA DARAJA


    Mabingwa wa Ligi Kuu, Simba SC

    KLABU ya African Lyon imenusurika kushuka daraja, baada ya kuifunga JKT Ruvu mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.
    Lyon imetimiza pointi 27 na kuungana na Polisi Dodoma, Villa Squad na Moro United kuiaga Ligi Kuu.
    Villa Squad jana iliifunga 2- 1 Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na kumaliza ligi na pointi 26 sawa na Toto Africans iliyofungwa bao 1-0 na Coastal Union jana Uwanja wa Mkwakwani Tanga.
    Mtibwa Sugar ilimaliza vizuri, baada ya kuifunga Moro United bao 1-0 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, hivyo Mtibwa kumaliza ligi ikiwa na pointi 42.
    Jana Simba ilitawazwa rasmi kuwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu, baada ya kuifunga Yanga mabao 5-0 na kumaliza ikiwa na pointi 62.
    Simba ilipata mabao yake kupitia kwa, Emmanuel Okwi dakika ya kwanza na Patrick na 65, Mafisango dakika ya 58 kwa penalti,
    Juma Kaseja kwa penalti pia dakika ya 69 na Felix Sunzu kwa penalti dakika ya 74.
    Wakati Simba ikimaliza na pointi zake 62, Azam imekuwa ya pili kwa pointi zake 56 baada ya jana kuifunga Kagera Sugar mabao 2-1 Uwanja wa Chamazi na Yanga imeshika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 49.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: POLISI DOM, VILLA, MORO ZASHUKA DARAJA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top