BONDIA ambaye hajawahi kupigwa katika ngumi za kulipwa, Floyd Mayweather ametoka jela juzi na anaonekana yuko fiti kabisa, mwenye afya njema na misuli ya nguvu baada ya kutoka ndani ya gereza la Clark County Jail, alikowekwa miezi miwili iliyopita. Bondia huyo sasa anaweza kupata ulingoni Novemba 8, mwaka huu kumaliza ubishi na mpinzani wake wa siku nyingi, Manny Pacquiao, pambano ambalo anaweza kulipwa dola za Kimarekani Milioni 200.
ANARUDI MTAANI: Floyd Mayweather akitolewa gerezani na walinzi kutoka gereza hilo la Las Vegas, baada ya kumaliza kifungo chake
TABASAMU LA UHURU: Mayweather akitabasamu wakati akilakiwa na marafiki na familia yake baada ya kutolewa jela |
Hii ni picha ambayo ameiweka kwenye twitter, cheki anavyoonekana |
0 comments:
Post a Comment