![]() |
| Coastal Union, wanaanza na Mgambo kesho |
Na Mahmoud Zubeiry
WAKATI Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 inaanza kutimua vumbi kesho, timu
zote 14 zikijitupa viwanja saba tofauti, kusaka pointi- hadi unaposoma habari hii,
klabu hazijapewa fedha zozote kutoka kwa wadhamini, hata za nauli na mbaya
zaidi, hata vifaa vya michezo havijatolewa.
Maana yake,
timu ambayo itashindwa kufika kituoni kesho kwa kigezo cha kutokuwa na fedha ya
nauli, itakuwa na haki na haitastahili adhabu yoyote, kwa sababu klabu nyingi
zinazoshiriki ligi hiyo hazina vyanzo vya mapato Azam FC, Simba na Yanga zenye ‘kujiweza’.
Habari zaidi
zinasema, hata marefa waliopangwa kuchezesha mechi za awali za ligi hiyo, hawajapewa
nauli za kwenda vituoni wala fedha za kujikimu, jambo ambalo linakaribisha
mazingira ya rushwa.
Refa atafikaje
kituoni? Akilini kiwachini mwake na akifika kwa hisani ya klabu atalaumiwa
akilipa fadhila?
Mabingwa
watetezi wa ligi hiyo, Simba wataikaribisha African Lyon kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam, wakati washindi wa pili wa ligi hiyo, Azam FC watakuwa
wageni wa Kagera Sugar, Uwanja wa Kaitaba, Bukoba na washindi wa tatu, Yanga
watakuwa wageni wa Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Mjini
Morogoro, Polisi Dodoma watakuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa
Jamhuri wakati jijini Tanga, Mgambo JKT ambayo imepanda daraja msimu huu
itaumana na Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
JKT Ruvu na
Ruvu Shooting zitapambana kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam
huku Azam ikiwatembelea Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Katiba.
Uwanja wa
CCM Kirumba jijini Mwanza utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Toto Africans dhidi
ya Oljoro JKT na mechi zote zitaanza saa 10.30 jioni.
Viingilio
katika mechi ya Simba na African Lyon vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya
kijani na bluu, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 viti vya VIP C
na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Viingilio kwa mechi nyingine vitakuwa sh.
3,000 na sh. 10,000.
Kwa ujumla
Ligi Kuu inaanza katika mazingira ya ubabaishaji wa hali ya juu- hali ambayo
lazima iepukwe ili kuboresha soka yetu.



.png)
0 comments:
Post a Comment