![]() |
| Obadia kushoto, akiwa na Mussa Mudde kulia. kama walijijua |
Na Mahmoud Zubeiry
TIMUA timua
imeendelea Simba SC na safari ni zamu ya beki Obadia Michael Mungusa. Beki huyo
wa zamani wa Mtibwa Sugar akiwa anaingia katika msimu wa pili kwenye klabu
hiyo, ametemwa.
Habari kutoka
ndani ya Simba SC, ni kwamba beki huyo ametemwa kwa zaidi ya mwezi mmoja,
ingawa inafanywa siri kwa kile ambacho viongozi wa klabu hiyo wanaelewa.
Lakini ajabu
Simba inamtema Obadia, wakati ina uhaba wa mabeki wa kati, kwani inao watatu
tu, Juma Nyosso, Paschal Ochieng na Komabil Keita, hali ambayo imefanya sasa
Shomary Kapombe ahamishiwe kwenye nafasi hiyo.
BIN ZUBEIRY ilimtafuta Obadia ambaye alisema
kwamba yeye anajitambua ni mchezaji halali wa Simba SC, kwa kuwa bado ana
mkataba na klabu hiyo wa mwaka mmoja zaidi, ila kwa sasa hayupo na timu kwa
kuwa anaumwa.
“Mimi nilikuwa
naumwa, viongozi wakawa hawaamini, nimecheza Kombe la Kagame naumwa, baada ya
mashindano, ikabidi niende Mwanza kujitibu, wao wakasema nisiondoke hadi
daktari anitazame, wakati ule daktari alikuwa hayupo, nikaamua kuondoka tu, kwa
sababu hali yangu ilikuwa mbaya.
Wakanipigia
simu kunihoji mbona umeondoka bila kuongea na daktari, ikabidi nirudi Dar es
Salaam, wakati huo timu inakwenda Arusha kambini, Daktari akaniambia niende kwa
daktari mmoja Dar es Salaam nikapimwe. Nilipoenda
kupimwa yule, daktari akasema kuna kipimo natakiwa kufanyiwa, akawasiliana na
viongozi, akawa anasubiri jibu. Ila wakawa wanamzungusha.
Mimi nikawapigia
simu viongozi kuwauliza, nikaambiwa ooh sijui sina mapenzi na timu mara wanasikia
eti nasema siwezi kwenda kambini kwa sababu nadai hela, kweli kuna haki zangu
nadai, lakini siwezi kugoma kufanya kazi kinyume na utaratibu, mimi ninaumwa. Basi
ndio hivyo, ikawa mabishano yakaishia hapo,”alisema Oba.
Hata hivyo,
kuhusu habari za kuachwa, Obadia anasema litakuwa jambo la alabu sana, kwa kuwa
awali yeye aliomba kuachwa baada ya msimu uliopita wa Ligi Kuu kumalizika, ili
atafute timu nyingine, lakini viongozi wakamkatalia.
“Nilipomaliza
ligi nilipata nafasi sehemu nyingine, mimi nilipokuwa Mtibwa nilikuwa nacheza. Nimekuja
Simba nikawa sichezi, nikawaambia viongozi, kama wanaona bado sina nafasi, bora
waniache niende. Wakaniambia nina mkataba siwezi kuondoka na kama kuna timu inanitaka
ije kuvunja mkataba.
Nikawoamba wanipeleke
sehemu hata kwa mkopo niwe nacheza, wakanihakikishia kucheza, kweli Kagame
imekuja nimeanza kucheza, bahati mbaya nikaumia, ndio nimekuja kujitibu sasa
yanaibuka haya tena, ila mimi bado ninajitambua ni mchezaji halali wa Simba,
kuwa kuwa nina mkataba,”alisema Oba.
Lakini kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alisema
anachofahamu kuhusu mchezaji huyo aliomba mwenyewe kurudi Mtibwa na kulingana
na taarifa yake ya uchezaji msimu uliopita, Kamati yake ikaafiki ombi hilo.
“Mimi nachofahamu
kutoka kwa uongozi, huyu mchezaji aliomba kurudi Mtibwa na kulingana na taarifa
yake ya uchezaji msimu uliopita, tukaridhia ombi lake,”alisema Hans Poppe.



.png)
0 comments:
Post a Comment