• HABARI MPYA

    Friday, June 14, 2013

    MAN CITY YAMTHIBITISHA PELLEGRINI KUWA KOCHA WAKE MPYA, YAMPA MKATABA WA MIAKA MITATU

    IMEWEKWA JUNI 14, 2013 SAA 1:16 USIKU
    KOCHA Manuel Pellegrini hatimaye ameteuliwa kuwa kocha wa Manchester City kwa Mkataba wa miaka mitatu na amesema kikosi chake kipya kitakuwa bora katika ligi. 
    Amewasili kutoka Malaga na kuchukua nafasi ya Roberto Mancini aliyefukuzwa baada ya matokeo mabaya msimu uliopita.
    Pellegrini amesema: "Nina furaha kukubali nafasi hii kubwa ya kuvutia. Klabu ina dira thabiti ya mafanikio ndani na nje ya Uwanja na ninajifunga kutoa mchango wangu muhimu,"alisema.
    Ready for action: Manuel Pellegrini says Man City have the best squad in the Premier League
    Tayari kwa kazi: Manuel Pellegrini amesema Man City ina kikosi bora katika Ligi Kuu ya England
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAN CITY YAMTHIBITISHA PELLEGRINI KUWA KOCHA WAKE MPYA, YAMPA MKATABA WA MIAKA MITATU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top