• HABARI MPYA

    Tuesday, June 11, 2013

    MAN UNITED YASAJILI MCHEZAJI WA KWANZA CHINI YA KOCHA MPYA MOYES, NI BEKI KINDA LA URUGUAY

    IMEWEKWA JUNI 11, 2013 SAA 3:24 USIKU
    BEKI wa pembeni, Guillermo Varela amekuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha mpya wa Manchester United, David Moyes. 
    DIli la kumsaini beki huyo mwenye umri wa miaka 20 wa kikosi cha Uruguay cha vijana chini ya umri wa miaka 20, kutoka klabu ya Penarol lilithibitishwa wiki iliyopita na amewasili Manchester kumwaga wino kwa mkataba wa miaka mitano leo.
    Getting shirty: Guillermo Varela poses with the new Manchester United kit after signing his five-year deal at the club
    Guillermo Varela akiwa na jezi ya Manchester United baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano
    Guillermo Varela
    Guillermo Varela

    Guillermo Varela amejiunga na Manchester United wakati David Moyes akianza mapinduzi Old Trafford

    "Nimefurahi sana kuwa sehemu ya klabu hii, moja ya timu bora duniani,"alisema Varela. Varela alifanya majaribio kwanza Old Trafford katika wiki za mwisho za msimu uliopita alivutia kiasi cha kuishawishi klabu iilipe Penarol Pauni Milioni 1.
    All smiles: Varela pets pen to paper on a five-year contract
    Varela akisaini Mkataba wa miaka mitano 

    Guillermo Varela ni nani?

    Alizaliwa Machi 24, mwaka 1993, mjini Montevideo, Uruguay 
    Aliichezea mechi ya kwanza Penarol Juni 2011, na haikuchukua muda akawa mchezaji wa kikosi cha kwanza katika beki ya kulia 
    Ameichezea mechi 10 timu ya taifa ya vijana ya Uruguay chini ya umri wa miaka 20, lakini bado hajachezea timu ya wakubwa
    "Kama ambavyo kila mmoja duniani anafahamu, hii ni klabu kubwa ambayo imeshinda kila kitu na kwa kweli ninatumai kuendelea hivyo,".
    "Nina bahari sana kuna watu wachache wanaozungumza Kispanyola hapa. Itanisaidia kutulia na kuweka mambo yangu sawa.'
    Varela muda si mrefu ataungana na U20 ya Uruguay kwa ajili ya Kombe la Dunia la FIFA la vijhana wa umri huo nchini Uturuki.

    VIDEO: Varela akifanya vitu


    New arrival: David Moyes will have Varela at his disposal after taking over as Manchester United manager
    Kocha mpya: David Moyes atakuwa na Varela Manchester United
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAN UNITED YASAJILI MCHEZAJI WA KWANZA CHINI YA KOCHA MPYA MOYES, NI BEKI KINDA LA URUGUAY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top