• HABARI MPYA

    Saturday, June 08, 2013

    PRISCA ATWAA TAJI LA MISS TANZANIA SINZA

    Mrembo aliyetwaa taji la Redd's Miss Sinza 2013, Prisca Element (katikati) akiwa na Mshindi wa pili Happynes Maira (kulia) na Mshindi wa tatu, Sarahy Paul, wakiwa na furaha mara baada ya kutangazwa washindi katika shindano lao lililokuwa likishikiliwa na Redd's Miss Sinza na Miss Tanzania 2012-2013, Brigitte Alfred
    Na Princess Asia, IMEWEKWA JUNI 8, 2013 SAA 4:00 USIKU 
    MREMBO Prisca Element juzi usiku alifanikiwa kumvua taji la kwanza Redd’s Miss Tanzania, Brigitte Alfred baada ya kufanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Sinza katika mchuano mkali uliofanyika ukumbi wa Meeda, uliopo Sinza Mori, Dar es Salaam.
    Brigitte mbali na kushikilia taji la Redd’s Miss Tanzania ndiye pia aliyekuwa mrembo wa Redd’s Miss Tanzania, hivyo kuvuliwa taji hilo la kwanza ni kudhihirisha kinyang’anyiro cha kumsaka mrithi wake kimeshika kasi.
    Katika shindano hilo lililokuwa kali na la kuvutia, huku burudani ikinogeshwa na kundi la African Stars ‘Twanga Pepeta’, nafasi ya pili ilichukuliwa na Happynes Maira na ile ya tatu akaitwaa Sarah Paul.
    Warembo wengine wawili waliofanikiwa kuingia katika tano bora walikuwa ni Nicole Michael na Nasra Hassan, ambao walitoa upinzani mkali katika shindano hilo lililokuwa likifuatiliwa kwa karibu na watu wengi.
    Akizungumza mara baada ya kufanikiwa kutwaa taji hilo, Prisca alisema ana uhakika mkubwa wa kufuata nyayo za Brigitte na kudai atahakikisha anaipigania Sinza kwa nguvu zake zote ili iweze kufanya vyema katika Redd’s Miss Tanzania.
    Brigitte alipoulizwa kuhusu shindano hilo na kuvuliwa kwake taji, alisema anaamini kwa dhati mrembo aliyechaguliwa atahakikisha kitongoji cha Sinza kinaendelea kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.
    “Kikubwa zaidi ni kujiamini na kufuata maelekezo unayopewa, lakini mrembo wetu naamini ana sifa zote zinazostahili na ni matumaini yangu atasonga mbele zaidi katika hatua inayofuata,” alisema.
    Redd’s Miss Tanzania kwa sasa inadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: PRISCA ATWAA TAJI LA MISS TANZANIA SINZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top