Na Princess Asia, IMEWEKWA JUNI 8, 2013 SAA 4:00 USIKU
MREMBO Prisca Element juzi usiku alifanikiwa kumvua taji la kwanza Redd’s Miss Tanzania, Brigitte Alfred baada ya kufanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Sinza katika mchuano mkali uliofanyika ukumbi wa Meeda, uliopo Sinza Mori, Dar es Salaam.
Brigitte mbali na kushikilia taji la Redd’s Miss Tanzania ndiye pia aliyekuwa mrembo wa Redd’s Miss Tanzania, hivyo kuvuliwa taji hilo la kwanza ni kudhihirisha kinyang’anyiro cha kumsaka mrithi wake kimeshika kasi.
Katika shindano hilo lililokuwa kali na la kuvutia, huku burudani ikinogeshwa na kundi la African Stars ‘Twanga Pepeta’, nafasi ya pili ilichukuliwa na Happynes Maira na ile ya tatu akaitwaa Sarah Paul.
Warembo wengine wawili waliofanikiwa kuingia katika tano bora walikuwa ni Nicole Michael na Nasra Hassan, ambao walitoa upinzani mkali katika shindano hilo lililokuwa likifuatiliwa kwa karibu na watu wengi.
Akizungumza mara baada ya kufanikiwa kutwaa taji hilo, Prisca alisema ana uhakika mkubwa wa kufuata nyayo za Brigitte na kudai atahakikisha anaipigania Sinza kwa nguvu zake zote ili iweze kufanya vyema katika Redd’s Miss Tanzania.
Brigitte alipoulizwa kuhusu shindano hilo na kuvuliwa kwake taji, alisema anaamini kwa dhati mrembo aliyechaguliwa atahakikisha kitongoji cha Sinza kinaendelea kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.
“Kikubwa zaidi ni kujiamini na kufuata maelekezo unayopewa, lakini mrembo wetu naamini ana sifa zote zinazostahili na ni matumaini yangu atasonga mbele zaidi katika hatua inayofuata,” alisema.
Redd’s Miss Tanzania kwa sasa inadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
MREMBO Prisca Element juzi usiku alifanikiwa kumvua taji la kwanza Redd’s Miss Tanzania, Brigitte Alfred baada ya kufanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Sinza katika mchuano mkali uliofanyika ukumbi wa Meeda, uliopo Sinza Mori, Dar es Salaam.
Brigitte mbali na kushikilia taji la Redd’s Miss Tanzania ndiye pia aliyekuwa mrembo wa Redd’s Miss Tanzania, hivyo kuvuliwa taji hilo la kwanza ni kudhihirisha kinyang’anyiro cha kumsaka mrithi wake kimeshika kasi.
Katika shindano hilo lililokuwa kali na la kuvutia, huku burudani ikinogeshwa na kundi la African Stars ‘Twanga Pepeta’, nafasi ya pili ilichukuliwa na Happynes Maira na ile ya tatu akaitwaa Sarah Paul.
Warembo wengine wawili waliofanikiwa kuingia katika tano bora walikuwa ni Nicole Michael na Nasra Hassan, ambao walitoa upinzani mkali katika shindano hilo lililokuwa likifuatiliwa kwa karibu na watu wengi.
Akizungumza mara baada ya kufanikiwa kutwaa taji hilo, Prisca alisema ana uhakika mkubwa wa kufuata nyayo za Brigitte na kudai atahakikisha anaipigania Sinza kwa nguvu zake zote ili iweze kufanya vyema katika Redd’s Miss Tanzania.
Brigitte alipoulizwa kuhusu shindano hilo na kuvuliwa kwake taji, alisema anaamini kwa dhati mrembo aliyechaguliwa atahakikisha kitongoji cha Sinza kinaendelea kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.
“Kikubwa zaidi ni kujiamini na kufuata maelekezo unayopewa, lakini mrembo wetu naamini ana sifa zote zinazostahili na ni matumaini yangu atasonga mbele zaidi katika hatua inayofuata,” alisema.
Redd’s Miss Tanzania kwa sasa inadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).