KOCHA Didier Deschamps amefungua kesi dhidi ya demu wa Samir Nasri aliyemtusi mwalimu huyo baada ya kutaja kikosi cha Ufaransa cha Kombe la Dunia bila kiungo huyo anayechezea Manchester City.
Anara Atanes aliposti kwenye Twitter- matusi haya; "F*** France and F*** Deschamps! What a s*** manager".
Lakini ingasa baadaye aliomba radhi, Deschamps atachukua hatua za kisheria dhidi ya Atanes.
Kituo cha Redio cha Ufaransa, RMC mimeripoti kwamba Deschamps na Shirikisho la Soka Ufaransa (FFF) wore wamefungua kesi dhidi ya Atanes, ambaye ni mzaliwa wa England na mwimbaji wa kundi la Pop, Fanfare.
0 comments:
Post a Comment