• HABARI MPYA

    Tuesday, December 04, 2012

    KOMBE LA UHAI KUANZA DESEMBA 7 KARUME

    Rais wa TFF, Leodegar Tenga

    Na Prince Akbar
    MICHUANO ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu za U20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 7, mwaka huu kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
    Michuano hiyo, ambayo hudhaminiwa na Azam, watengenezaji na wasambazaji wa maji ya Uhai, inatarajiwa kufikia tamati Desemba 22 mwaka huu.
    Ofrisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY mjini hapa kwamba, wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ni wale tu ambao usajili wao umefanyika TFF na kupatiwa leseni.
    “Hakutakuwa na usajili mwingine wowote mbali na ule uliofanyika sambamba na wa Ligi Kuu. Taratibu zote za michuano hiyo zitafahamishwa kwa klabu husika ikiwemo ratiba ya michuano hiyo,”alisema ‘Big Bon’.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KOMBE LA UHAI KUANZA DESEMBA 7 KARUME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top