• HABARI MPYA

    Tuesday, December 11, 2012

    UMONY AANGUKA AZAM, SIMBA WAISHIA KUNAWA

    Brian Umony, kifaa kipya Azam 

    Na Mahmoud Zubeiry
    MSHAMBULIAJI wa Uganda, Brian Umony ametua Azam FC ya Dar es Salaam kwa mkataba wa miaka miwili, akitokea KCC ya kwao, Uganda.
    Awali, Umony alifanya mazungumzo na Simba SC ya Dar es Salaam pia na kufikia nao makubaliano, lakini Wekundu hao wa Msimbazi kwa kitendo cha kuchelewa kumalizamna naye, sasa ‘wanaishia kunawa’.
    Umony alikuwa pia akiwaniwa na El Merreikh ya Sudan, ambayo nayo ilituma mwakilishi wake kwenda kuzungumze naye Uganda wiki iliyopita.
    Brian amerejea nyumbani Uganda na kujiunga na KCC baada ya kumaliza mkataba wake, Becamex Binh Duong F.C. ya Vietnam.
    Mwaka 2009, baada ya Simba kuzidiwa kete na SuperSport United ya Afrika Kusini, ikamsajili Emmanuel Okwi aliyekuwa SC Villa wakati huo.
    Umony aliichezea Supersport United hadi 2010 alipohamia University of Pretoria ya Afrika Kusini pia hadi mwaka 2011 alipohamia Portland Timbers ya Marekani kwa mkopo na mwaka huu akatua Becamex Binh Duong F.C. Brian anang’ara katika Kombe la Challenge, hadi sasa ana mabao matatu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: UMONY AANGUKA AZAM, SIMBA WAISHIA KUNAWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top