MALINZI AREJESHA FOMU YA KUOMBA URAIS TFF, ALICHUKUA KWENYE MTANDAO
Mwenyekiti wa Chama cha Soka Kagera (KRFA), Jamal Emil Malinzi akirejesha fomu ya kugombea urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ofisi za shirikisho hilo, Ilala, Dar es Salaam mida hii, kuelekea uchaguzi utakaofanyika Februari 24, mwaka huu mjini Dar es Salaam. Anayepokea fomu hiyo ambayo Malinzi alichukua kwenye tovuti ya TFF na kujaza kisha kuilipia katika benki ya CRDB kushoto ni Ofisa wa TFF, Jonathan Aloyce Kakwaya.