SIRI ya mshambuliaji wa kimataifa wa
Uganda, Emmanuel Arnold Okwi kujituma na kuwa nyota wa mchezo dhidi ya watani
wa jadi, Simba SC ni ahadi nono aliyopewa na mfadhili wa zamani wa klabu hiyo,
Azim Hussein Hasham Dewji (pichani kushoto), BIN ZUBEIRY imeipata hiyo.
Habari kutoka ndani ya Simba SC, zimesema
kwamba wakati timu hiyo inaingia kwenye mchezo dhidi ya watani hao wa jadi, Yanga-
hofu yao ilikuwa juu ya Okwi mshambuliaji ambaye pamoja na makali yake, awali
tangu ajiunge na timu hiyo miaka mitatu iliyopita, hakuwahi kutikisa nyavu za
Yanga.
Lakini mchezo wa Mei 6, 2012 kwa kujua kabisa
yeye ni tegemeo la timu hiyo, aliwekewa mikakati mizito ili siku hiyo acheze
soka yake yote na kuibeba timu.
“Ilibidi Dewji, ambaye kwa kweli hivi sasa
anaisaidia sana SImba ingawa tu hajitangazi, akae naye na kumpa ahadi nono,
alimuambia kila bao analofunga anampa Milioni moja. Na kila pasi ya bao anampa 500,000.
Sasa amekula fedha ya mabao mawili ya
kufunga na zile penalti mbili alizosababisha inakuwa sawa na pasi za mabao. Na Dewji
alimpa fedha zake zote siku ile ile baada ya mechi,”kilisema chanzo chetu
kutoka Simba SC.
Katika siku za karibuni, Dewji amekuwa
akiisaidia mno Simba, na hiyo inatokana na umoja aliourejesha Mwenyekiti wa
klabu hiyo, Alhaj Ismail Aden Rage kwenye klabu hiyo tangu aingie madarakani,
kwani hata kundi la Friends Of Simba nalo linasaidia timu sasa.
Dewji ni mfadhili wa kihistoria ndani ya
SImba, ambaye ana mchango mkubwa mno kwenye mafanikio ya kihistoria ya klabu
hiyo.
Juhudi zake ndizo ziliipa SImba mataji manne
ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, sasa Kombe la Kagame, katika miaka ya
1991, 1992, 1995 na 1996 na mwaka 1993 aliiwezesha klabu hiyo kufika fainali ya
Kombe la CAF.
![]() |
| Okwi |
Lakini kutokana na migogoro, mwaka 1996
Dewji alijitoa na SImba kuinunua iliyokuwa SIgara SC, ambayo hata hivyo
ilishushwa Daraja la FAT kwa kosa la kumtumia kipa Manyika Peter bila kukamilisha
taratibu za uhamisho wake kutoka Mtibwa Sugar.
Baadaye Sigara ilinunuliwa na Mtanzania
anayeishi Marekani, Alexander Otaqs Kajumulo na tangu hapo, Dewji alibaki kama
mdau wa kawaida wa soka.
Lakini katika kipindi chote hicho
ameendelea kusaidia soka.
Bado Dewji huwezi kumtenganisha na
mafanikio ya timu ya taifa ya Bara kutwaa Kombe la Challenge mwaka 1994 nchini
Kenya, kwani yeye ndiye aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya timu.
Dewji ambaye amewekeza hadi nchini Zambia,
timu ya taifa ya nchi hiyo< chipolopolo ilipotwaa Kombe la Mataifa ya
Afrika, mapema mwaka huu aliizawadia pia.
Mwaka juzi, alikuwa miongoni mwa
Wakurugenzi wa Moro United, ambayo hata hivyo baadaye alijitoa kutokana na
kujitokeza watu wenye mlengo wa kushoto.
![]() |
| Okwi akimburuza Nsajigwa |
Hivi karibuni, Dewji amemwaga mamilioni
kibao kumsajili Simba kiungo baab kubwa, Nizar Khalfan aliyekuwa akicheza soka
ya kulipwa Marekani, katika klabu ya Simba.




.png)
0 comments:
Post a Comment