• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    MAKELELE AMTANDIKA MKE WAKE, AMJERUHI VIBAYA


    Thandi Ojeer and Claude Makelele
    ENZI ZA RAHA ZAO;  Thandi Ojeer na Claude Makelele kabla ya kuachana

    Thandi Ojeer
    Thandi baada ya kujeruhiwa
    MLIMBWENDE wa Kiingereza, alijikuta anapoteza uzuri wa sura yake baada ya kutandikwa makonde usoni na nyota wa zamani wa klabu ya Chelsea ya England, Claude Makelele, Mahakama imesema jana.
    Thandi Ojeer, mwenye umri wa miaka 35 — ambaye aliishi na Mfaransa huyo kwa miaka miwili — alipigwa na kuumizwa vibaya na kiungo huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa.
    Kwa sababu hiyo anataka kulipwa fidia ya pauni 70,000 kutoka kwa mchezaji huyo wa zamani wa Real Madird, mwenye umri wa miaka 39.
    Ugomvi huo uliotokea nyumbani kwa mchezaji huyo mwaka 2010 Jijini Paris, ambako kwa sasa anaifundisha klabu ya Paris Saint-Germain.
    Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi iliyosomwa katika mahakama ya Versailles Correction, Ojeer aliingia nyumbani kwa mchezaji huyo baada ya kukuta geti liko wazi. Makelele, ambaye hakuwapo mahakamani, alisema kwa kitendo hicho alishambuliwa vikali usoni na kujeruhiwa.
    Ms Ojeer, mkazi wa London-ambaye ni muandaaji wa shughuli, alihudhuria sherehe kadhaa na Makelele katika Paris Fashion Week, lakini hakuna maelewano baina yao.
    Lakini Mwanasheria wa Ojeer, alisema Makelele alimpiga mteja wake. Stanislas Panon alisema mteja wake alihitaji tiba makini hospitali kwa majeruhi aliyopata, ikiwemo jino na alilazimika kuwa nje ya kazi.
    Wakili wa Makelele alisema kwamba “Alikuwa anajaribu kumtoa nje ya nyumbani kwake, lakini katika kugoma wakagombana”.
    Kiungo huyo hodari wa zamani, aliwaambia Polisi kwamba alikwishaachana na mwanamke huyo na hakutaka tena kumuona nyumbani kwake. Mwanamke huyo alisema alikwenda kuchukua nguo zake. Kesi hiyo imeahirishwa hadi mwezi ujao.
    Mwanamke mwingine wa zamani wa Makelele, mwanamitindo wa M&S, Noemie Lenoir, alijaribu kujiua mapema mwaka 2010.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAKELELE AMTANDIKA MKE WAKE, AMJERUHI VIBAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top