• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    HODGSON ATEUA KOCHA WA MAKIPA ENGALND


    Dave Watson

    KOCHA mpya wa timu ya soka ya taifa ya England, Roy Hodgson ameanza kutengeneza benchi lake la ufundi, kwa kumteua kipa wa makocha wa Birmingham City, Dave Watson kufanya kazi hiyo katika timu ya taifa kwa ajili ya fainali za mwezi ujao za Kombe la Mataifa ya Ulaya.
    England pia inataka kumrejesha kipa wa zamani wa Liverpool na England, Ray Clemence, aliyekuwa kocha wa makipa wakati wa Fabio Capello afanye kazi na Hodgson.
    Watson, pia alifanya kazi kwa karibu na Joe Hart wakati kipa huyo namba moja wa sasa wa England alipokuwa akicheza kwa mkopo Birmingham msimu wa 2009/2010.
    Mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha vijana cha England chini ya umri wa miaka 21, Watson alichezea klabu ya Barnsley enzi zake, ingawa alilazimika kustaafu akiwa ana umri wa miaka 28 tu, baada ya kuumia.
    Hodgson, anayetarajiwa kutaja kikosi chake cha Euro 2012, wiki ijayo katika michuano itakayofanyika Poland na Ukrine, alimkaribisha Watson kwa kusema: "Dave ana thamani kubwa katika mchezo na anaheshimika sana mbele ya makipa waliofanya naye kazi, muhimu Joe Hart.
    "Amefanya kazi na makipa wengi wa England na ana uzoefu wa kufanya kazi za maendeleo ya timu, hivyo tunafahamu atafaa sana kwenye kikosi.
    "Binafasi nafurahi kuwa naye kama sehemu ya benchi la ufundi la England kwenye michuano hiyo. Ningependa kuwashukuru wote katika klabu ya Birmingham City kwa kumkubalia Dave kufanya kazi katika Euros."


    Print mail del.icio.us Reddit Digg Twitter Facebook StumbleUpon
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HODGSON ATEUA KOCHA WA MAKIPA ENGALND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top