• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    MSAIDIZI WA WENGER AACHIA NGAZI ARSENAL


    Pat Rice
    Rice
    KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amemsifu msaidizi wake katika klabu hiyo, Pat Rice, ambaye ataondoka mwishoni mwa msimu huu, baada ya miaka 44 akiwa na 'Gunners'.
    Mrithi wake atakuwa ni mlinzi wa zamani wa Arsenal, Steve Bould. Rice, ambaye aliichezea Arsenal katika mechi zaidi ya 500, alijiunga na wafanyikazi wa klabu ya Arsenal mwaka 1996, wakati Mfaransa Arsene Wenger alijiunga na klabu kama meneja.
    Kama meneja msaidizi, Rice aliisaidia Arsenal kufanikiwa kupata ushindi wa ligi ya Premier mara tatu, na mara nne kulitwaa Kombe la FA.
    Meneja Wenger amesema ni vigumu kukadiria kazi aliyoifanya Rice, na kuelezea kwamba ni jambo la "huzuni, huzuni, huzuni sana, na binafsi namshukuru kwa mchango wake katika kunisaidia wakati wangu na ningependa anisamehe kwa baadhi ya shida alizozipata katika kipindi alichokuwa chini yangu, lakini alikuwa ni msaidizi mwaminufu sana, na ninamshukuru kwa kuwa kando yangu kwa muda mrefu hivyo".
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MSAIDIZI WA WENGER AACHIA NGAZI ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top