• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    YAYA TOURE ATAKA MAKUBWA MAN CITY


    Yaya Toure
    Yaya Toure

    Yaya Toure
    Yaya Toure

    KIUNGO wa kimatairfa wa Ivory Coast, Yaya Toure amesema kwamba anataka kuisadia klabu yake ya Manchester City iwe klabu bora duniani.
    Mwanasoka huyo bora wa mwaka Afrika, amekua chachu ya mafanikio ya klabu hiyo msimu huu, ambayo Jumapili inatarajiwa kuhitimisha kwa msimu kwa taji la Ligi Kuu ya England.
    Yaya amesema; “Sababu iliyonileta hapa ni kuisadia timu.......kusaidia katika kuipeleka mbele na kuifanya iwe kubwa kuliko zote duniani,”alisema.
    City itakuwa mwenyeji wa QPR Jumapili na ikishinda mechi hiyo itakuwa bingwa- labda Manchester United iifunge Sunderland kwa angalau mabao 10-0.
    Alipoulizwa kama ameanza kuhisi shinikizo za pambano hilo la mwisho, Toure aliyesajiliwa kutoka Barcelona kwa kitita cha pauni milioni 24, alijibu hapana, kwa sababu nina uzowefu. Nimeisha shiriki michuano kama hii na kushinda vikombe kadhaa.
    Toure, alikua na klabu ya Barcelona iliyoshinda vikombe sita vya nchini na nje ya nchi mwaka 2009 na amekua kishawishi kikubwa msimu huu kwa Manchester city.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YAYA TOURE ATAKA MAKUBWA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top