• HABARI MPYA

    Thursday, May 03, 2012

    MECHI YA SIMBA NA YANGA YAAHIRISHWA, AZAM NA MTIBWA KURUDIANA KESHO TAIFA


    Kiiza wa Yanga kushoto akitafuta mbinu za kumtoka Nassor Masoud Chollo wa Simba katika mechi iliyopita baina ya timu hizo, miamba hiyo sasa itacheza Jumapili badala ya Jumamosi.

    KIKAO cha Kamati ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bata leo kimepanga mechi kati ya Azam na Mtibwa Sugar ichezwe kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, iliyokuwa ifanyike Jumamosi sasa imesogezwa mbele hadi Jumapili.
    Azam na Mtibwa Sugar wanarudiana kesho jioni Uwanja wa Taifa, kufuatia maamuzi ya Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya Mwenyekiti wake Alfred Tibaigana jana.
    Kamati ya Tibaigana, Kamanda Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Kanda Maalum, Dar es Salaam, jana ilibatilisha maamuzi ya Kamati ya Ligi Kuu, kuipa Azam ushindi, baada ya kuvunjika mechi yao na Mtibwa wiki iliyopita, zikiwa zimebaki dakika chache mchezo kumalizika na kuamuru mechi irudiwe.
    Kamati ya Tibaigana ilibaini mapungufu kwa marefa wa mechi hiyo, kwani hawakufuata kanuni za mchezo kusubiri kwa dakika 10 kabla ya kumaliza mechi hiyo, baada ya Mtibwa Sugar kugomea penalti timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1.
    Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Wallace Karia ameiambia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba kwa sababu walipanga mechi zote za mwisho za ligi zichezwe siku na wakati mmoja Jumamosi, kutokana na Azam na Mtibwa kuwa na mechi kesho, hawataweza kucheza siku mbili mfululizo.
    Kwa sababu hiyo, Karia amesema Kamati imeamua mechi za mwisho zote, ikiwemo ya watani wa jadi Simba na Yanga sasa zichezwe Jumapili, ili kuzipa nafasi ya kupumzika siku moja Azam na Mtibwa kabla ya kuingia kwenye mechi zao za mwisho.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECHI YA SIMBA NA YANGA YAAHIRISHWA, AZAM NA MTIBWA KURUDIANA KESHO TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top