• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    MESSI APATA KASHFA NZITO YA UBAGUZI


    Royston Drenthe vs Lionel Messi, Hercules - Barcelona
    Drenthe kushoto akizinguana na Messi
    WINGA wa Everton, Royston Drenthe amemshushia shutuma nzito, Mwanasoka Bora wa Dunia mara tatu, Lionel Messi, akidai kwamba nyota huyo wa Barcelona alimuita 'negro' (mtu mweusi) zaidi ya mara moja uwanjani.
    Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Uholanzi, alikutana uwanjani mara kadhaa na Muargentina huyo wakati akichezea Real Madrid na Hercules, na amesema wakati wote alikuwa anakwaruzana na Messi akiwa hana mpira.
    "Tumecheza sana tu dhidi yake, na wakati wote tulikuwa tunazinguana. Unajua nini kinachonisumbua sana mimi? Ile sauti ambayo ainiita 'negro, negro'," Drenthe alisema kwenye mahojiano na jarida la Helden la Uholanzi.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, Drenthe kwa sasa anachezea Everton ya Ligi Kuu England kwa mkopo na anapenda kuhamia moja kwa moja katika klabu hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI APATA KASHFA NZITO YA UBAGUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top