• HABARI MPYA

    Monday, May 07, 2012

    SAMATTA ATUPIA TENA MAZEMBE IKIUA 6-0, AENDA NA SIMBA SUDAN



    MSHAMBULIAJI chipukizi wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ‘Sama Goal’ ameendeleza makali yake ya kufunga mabao katika klabu yake ya Tout Puissant Mazembe, baada ya jana kuichapa mabao 6-0 Elima katika Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    Katika mchezo huo, uliofanyika kwenye Uwanja wa Frederic Kibassa Maliba, Lubumbashi, mshambuliaji mpya wa Mazembe, Hope Traore kutoka Mali alifunga mabao matatu peke yake, akiichezea mechi ya kwanza klabu hiyo.
    Mbali na bao la Samatta, mabao mengine ya Mazembe yalitupiwa kimiani na Kanda Lungu na Sinkala Tusilu.
    TPM sasa inaongoza ligi kwa wastani wa pointi mbili dhidi ya Vita Club inayoshika nafasi ya pili, 19-17.
    Mazembe wanatarajiwa kuondoka kesho kwenda Khartoum, Sudan tayari kwa mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya El Merreikh kwenye Uwanja wa Omduran.
    Mazembe ilishinda 2-0 mechi ya kwanza na huko inahitaji sare ili kusonga mbele.
    Ikiwa huko, Samatta na mchezaji mwenzake wa zamani wa Simba, Patrick Ochan, watakutana na timu yao hiyo ya zamani, ambayo mwishoni mwa wiki hii inacheza na Al Ahly Shandy katika mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho.
    Simba yenyewe inahitaji sare pia, baada ya ushindi wa awali 3-0 nyumbani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA ATUPIA TENA MAZEMBE IKIUA 6-0, AENDA NA SIMBA SUDAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top