 |
Manji akiwa amemuinua mkono Bin Kleb, wengine kulia ni Manyama na Nyambaya, wakati kushoto ni Sanga |
Na Mahmoud Zubeiry
MGOMBEA Uenyekiti wa klabu ya Yanga, katika uchaguzi wa
Jumapili ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Yussuf Mehboob Manji leo
ametambulisha watu watano anaotaka kuchaguliwa nao wakati alipokuwa akihutubia mamia
ya wanachama kwenye Mkutano wa kampeni, Uwanja wa Kaunda, uliopo makao makuu ya
klabu, makutano ya Mitaa ya Twiga na Jangwani.
Manji aliwataja watu hao kuwa ni nafasi ya Makamu
Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wanne ni Abdallah Bin Kleb, Mussa Katabaro,
Lameck Nyambaya na George Manyama.
Ikumbukwe uchaguzi huo mdogo unafuatia Wajumbe wengi wa Kamati
ya Utendaji iliyochaguliwa miaka miwili iliyopita, akiwemo Mwenyekiti Wakili
Lloyd Baharagu Nchunga na Makamu wake, Davis Mosha kujiuzulu na
watakaochaguliwa Jumapili watadumu kwa miaka miwili, kumalizia kipindi cha
uongozi cha waliojiuzulu.
Manji aliwaomba wanachama wa Yanga pamoja na kumchagua yeye
Jumapili, pia wawachague na watu hao watano, Sanga, Katabaro, Bin Kleb,
Nyambaya na Manyama, kwani ni watu ambao anaamini atafanya nao kazi vizuri na
kwa ufanisi.
Alisema iwapo akichaguliwa watu hao na mambo yakawa mabaya
klabuni, atakuwa tayari kujiuzulu lakini akasema atasikitika iwapo atachaguliwa
pamoja na watu tofauti nao hao.
Alisema katika kipindi hiki ambacho klabu haina uongozi,
watu hao watano wamekuwa wakimsaidia kujenga timu kama kusajili na kadhalika
kwa kujitolea hivyo ana imani nao kwa kiasi kikubwa.
Shughuli hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa wanachama Vijana
wa Yanga, Bakili Mohamed Makele na Mwenyekiti wa Wazee, Mzee Ibrahim Ally
Akilimali, ambao waliwaomba wana Yanga kuchagua timu hiyo na mambo yatakuwa
mazuri.
Umati wa wanachama wanaokadiriwa kufika 2000 au zaidi
ulihudhuria mkutano huo na wakati wote walikuwa wakishangilia hotuba, kuonyesha
kwamba wanaafiki.
 |
Manji anahutubia |
 |
Manji anahutubia |
 |
Manji anahutubia |
 |
Manji anahutubia kwa hisia kali |
 |
Manji anahutubia kwa msistizo |
 |
Mwenyekiti mtarajiwa Yanga |
 |
Mtu wa kazi, Bin Kleb |
 |
Pentagon inavyoonekana |
 |
Hapa anasema baada ya mwaka mmoja tu wa kuwa madarakani; Yanga itakuwa zaidi ya TP Mazembe |
 |
Manji inabidi ajenge na vyoo uwanjani akichaguliwa; Mzee huyu alishikwa wakati mkutano ukiendelea, akaamua kujisitiri hapa |
 |
Kura za Manji, Sanga, Bin Kleb, Manyama na Nyambaya zikijipoza kwa uji wa mchele |
 |
Watu wanapiga makofi; maana yake jeshi limekubalika |
 |
Mussa Katabaro anamwaga sera |
 |
Bin Kleb anamwaga sera, alisema yeye si mtu wa maneno, ni mtu wa vitendo |
 |
Nyambaya anamwaga sera |
 |
Kachaa anapiga mzigo wakati mkutano unaendelea |
 |
Sanga kushoto akimsalimu Bin Kleb. Katikati ni Katabaro |
 |
Akina mama nao watampa Manji na timu yake, kura zao |
 |
Manji akipongezana na jembe lake, Bin Kleb |
 |
Hapa aanahidi kulipa kisasi cha 6+5= 11 |
 |
Kwa kuingia mkutanoni ilibidi uwe na kadi ya uanachama, basi wasio na kadi waliishia kupiga chabo |
 |
Kampeni zinaendelea kwenye mkutano |
 |
Nyomi |
 |
Ibada zinaendelea sambamba na kusikiliza hotuba za kampeni |
 |
Nyomi |
 |
Rais na Makamu wake wakijadiliana |
 |
Nyomi |
 |
Mzee Akilimali akiwaombea kura vijana kwa hisia zote |
 |
Rais na Makamu wake wakijipanga mapemaa |
 |
Manji anamwaga sera |
 |
Hamisi Kiiza 'Diego' akiondoka baada ya kusikiliza kampeni |
0 comments:
Post a Comment