• HABARI MPYA

    Tuesday, August 14, 2012

    AKUFFO APEWA MKATABA, MUDDE APONA, OCHIENG HAKIJAELEWEKA

    Mussa akipangua msitu wa mabeki
    AMEPONA. Kiungo Mganda, Mussa Mudde hatatemwa tena na badala yake, beki Paschal Ochieng ili kujua hatima yake kusajiliwa au kutosajiliwa Simba SC, atasubiri wachezaji wawili wanaokuja kutoka Mali na mmoja kutoka Ivory Coiast.
    Hivi sasa Simba SC inatayarisha mkataba kwa ajili ya mshambuliaji Daniel Akuffo kutoka Hearts Of Oak ya Ghana ambao utapelekwa Arusha, timu hiyo ilipoweka kambi ausaini.
    Habari kutoka Arusha, ambako Simba imeweka kambi kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu, zimesema kwamba katika siku ya kwanza ya mazoezi yao na kikosi hicho leo, wachezaji wote hao wawili wameonyesha viwango vya hali ya juu.
    Imeelezwa kwamba, mshambuliaji Akuffo ni hatari mno na kwa haraka haraka hakuna wa kumfananisha naye kati ya washambuliaji wote waliopo Tanzania kwa sasa.
    Anasifiwa kuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, kasi, nguvu, ufundi na mbinu za kimchezo- maana yake Wekundu wa Msimbazi wamelamba dume.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AKUFFO APEWA MKATABA, MUDDE APONA, OCHIENG HAKIJAELEWEKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top