• HABARI MPYA

    Monday, August 06, 2012

    AZAM: SIMBA WAMEKURUPUKA KUMSAJILI REDONDO, WAMEPOTEZA FEDHA ZAO BUREE


    Na Mahmoud Zubeiry
    AZAM FC imesema kwamba, Simba SC imekurupuka kumsajili kiungo Ramadhani Suleiman Chombo ‘Redondo’, bila kuwasiliana na klabu yake na yatawatokea kama yaliyowatokea kwa Ibrahim Rajab ‘Jeba’, kupoteza fedha zao walizompa mchezaji.
    Kiongozi mmoja wa Azam, ameiambia BIN ZUBEIRY sasa hivi kwamba, wanasikia tetesi  leo Redondo amesajiliwa Simba SC, lakini mchezaji huyo bado ana mkataba na Azam hadi Juni mwakani.
    “Redondo alikuwa hajui mkataba wake unamalizika lini Azam, alinifuata kuniomba nimuongezee fedha asaini mkataba mpya, nikamuahidi nitafanya hivyo, lakini baadaye nakuja kugundua mkataba wake unaisha Juni mwakani, nikamuambia asubiri angalau baada ya miezi miwili.
    Kwa sababu haiwezekani umpe mtu fedha wakati mkataba wake bado muda mrefu kiasi hiki, sasa ajabu amekwenda kusaini Simba, “alisema kwa kustaajabu kiongozi huyo.
    Habari za uhakika kutoka kwa Wekundu hao wa Msimbazi zimeithibitishia BIN ZUBEIRY kwamba Redondo amesaini Simba. Kiungo huyo aliyejiunga na Azam mwaka 2009, akitokea Simba anakuwa mchezaji wa pili ndani ya kipindi kisichozidi siku tano kutua Msimbazi, akitokea Azam, baada ya Jumatano iliyopita, Mrisho Ngassa pia kusajiliwa na timu hiyo akitokea Chamazil.
    Alipoulizwa Ofisa Habari wa Smba SC, Ezekiel Kamwaga alisema kwamba hawezi kuzungumzia suala hilo kwa sasa.
    Simba ilimsajili mshambuliaji chipukizi wa Azam, Jeba aliyekuwea akicheza kwa mkopo Villa Squad kwa kuamini hana mkataba na klabu yake, lakini baadaye ililazimika kumsalimisha mchezaji huyo baad aya kugundua ana mkataba na Azam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM: SIMBA WAMEKURUPUKA KUMSAJILI REDONDO, WAMEPOTEZA FEDHA ZAO BUREE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top